Pages

Saturday, November 8, 2014

JE UNAIJUA AINA ZA STYLE ZA KUNYOA ZA SHETANI?
NA WANADAMU WANAINYOA?

SOMA HAPA….

Aina za kunyoa nywele ya kuzimu, ambayo ndiye majini yanayonyoaga cha ajabu niliona kuzimu na aina hizi za minyweo alizibuni jini Abubakari ili kuhakikisha tu kwa kila njia shetani aweze kuwateka wanadamu pale tu mtu anapofanya kitu cha kuzimu tayari na yeye anakuwa wa kuzimu sasa maji siku zote yanafuata mkondo, hayaendi mahali pasipo na njia hivyo hivyo na mwanadamu na yeye anapoiga kunyoa style za shetani basi anayafungulia majini yamfuate alipo na yanamkontrol maisha yake na kukufanya wewe ni wa kuzimu na hauendi mbinguni. Ameitumia njia hii pia ili pale MUNGU atakapo kukuchukua wakati wa unyakuo isiwezekane haijalishi umeokoka na unaishi maisha matakatifu, tayari unakuwa kichwa chako ni cha jini katika ulimwengu wa roho na kukuzuia usifike mbinguni, na zaidi majini yanakuwekea tabia zao mfano ulevi, ugomvi, wizi, ufisadi, kupenda miziki ya kidunia na umalaya. Na hata wewe chunguza utaona asilimia kubwa ya watu wenye kunyoa style za ajabu tabia zao zinafanana.

AINA ZA STYLE ZA MAJINI WANAZINYOA

1.     KIDUKU- ina maana upande wa kulia ni dunia imekutawala na upande wa kati kati penye nywele ni shetani amekaa kati kati yako wewe uliyenyoa na upande wa kushoto ulio hauna nywele na ni dunia imekushika.

2.     KISAHANI- ina maana katika kichwa chako uliyenyoa hivyo juu ya kichwa chak shetani amejenga mji wake, kule kuzimu mji wa jka kuu unaitwa Freeman Village na ramani yake ni ya duara (kisahani  style) hapo juu ya kichwa chako ni mji wake.

3.     PUNK ZOTE- aina zote za punk ni style za jini anayeitwa makata yeye peke yake ndie anayenyoa style hii, hivyo unaponyoa na wewe unafungulia urafiki majini makata wakufuate na kuharibu maisha yako na kisha hata unapokata roho hawa makata huja kuichukua sababu na wewe katika ulimwengu wa roho unaitwa makata japo hapa ulimwenguni unaitwa fulani.

4.     KUNYOA NYWELE ZOTE HALAFU UNAWEKA KIBWENZI- aina hii unakuwa umenyoa aina ya mnyoo wa tumbili (velvet monkey) hivyo katika ulimwengu wa roho na wewe unaitwa tumbili na tabia za tumbili zinakufuata ikiwemo tabia zake kubwa ni uzinzi na uwizi na utapeli.

5.     KUANDIKA CHOCHOTE KATIKA KICHWA- unapoandika chochote katika kichwa au umeweka alama yeyote ile ni dhambi, pili kila unachoandika unakuwa umejiandika jina la jini lililopo kuzimu, iwe umeandika hata kama jina lako iwe ni kwa mkasi au ni kwa kupiga rangi, hapo tayari unakuwa umejitenga na MUNGU usiende mbinguni, huu ni mtego wa shetani japo unampenda MUNGU lakini unapigwa upofu, sasa mshukuru YESU aliyenituma mimi Hebron niwaeleze ukweli wa habari njema ili mpone. Na shetani alichokifanya hawa  wanaoandika vichwani majina huwapa majini ya kuwapa umaarufu, ila sasa hakuna tena huo umaarufu wa shetani kufanya kazi hapa ulimwenguni. Nimekwisha bomoa na mtaona haya ninayowaeleza uyaonapo usishangae ukumbuke ujumbe huu niliokuletea Nabii Hebron Kisamo, ingia www.prophethebron.blogspot.com usome zaidi na vitabu vyangu.

AINA ZA KUNYOA NDEVU (STYLE ZA KUZIMU)

1.     O style- unakuwa unajini linaitwa Abubakari (Sharubaro).
2.     Kuchora chini ya kidevu staili yeyote- jini Makata.
3.     Kupaka ndevu dawa iwe njano, nyekundu, yeyote  ile (Abubakar jini).
4.     Kuwa na nywele (ndevu) ndefu zinazogusa hata sehemu ya chakula (unakuwa wewe ni beberu wa kuzimu).
5.     Kunyoa ndevu kama style za mbuzi- uelewe tayari unalo jini ndani yako (je na wewe unanyoaje ndevu?)

NOTE:
Kila anayenyoa staili hizi ajielewe katika ulimwengu wa roho yeye amekuwa ni shoga ameolewa na hayo majini na inawezekana haujui lakini mshukuru YESU WA NAZARETI aliyeniokoa mimi Hebron kwa ajili ya kufanya kazi yake, watu wamjue MUNGU na wasije wakachomwa moto, niwafunulie siri za shetani ili asiweze kuwatega tena na niwafunulie siri za ufalme wa MUNGU ili mwende mbinguni na giza liondoke, sababu giza linatanda katika idadi kubwa watu hawajui na huko ndiko kutekwa na shetani na kanisa limemsaliti YESU kupitia watumishi wao wanaofanya biashara sasa wameamua kuitenda dhambi na hawasemi ukweli 98% na ndio sababu hata hii minyweo ya shetani ikaingia katika ulimwengu wote sababu YESU hakumpata wa kumueleza na kumuonyesha haya ili watu wasifanye na hadi kutekwa, na cha ajabu hata ukiangalia style za watumishi wanazinyoa utaona nao wengi wao wamenyoa aina hizi hizi na kama wananyoa aina hii hii ina maana na watumishi wa jinsi hiyo nao wameolewa na majini katika ulimwengu wa roho, na kama ameolewa na majini je unatazamia uipate injili yenye YESU wa kweli? Au atakuwa anamuaga maroho machafu katika kanisa, na kanisa kuwa ni watenda uchafu, ufisadi (wametekwa na shetani).

Ukikuta mtumishi ametoboa masikio anavaa hereni halafu anawahubiria injili ya YESU, elewa huyo ni shoga katika ulimwengu wa roho na hata awe ni mwanaume yeyote yule ajielewe ameolewa na jini, sasa amua leo uitupe hiyo herein ili mahusiano yako ya kuolewa na jini yaishe uokoke upya. Pia nataka muelewe katika nchi nyingi watu wanasema mashoga wanaoonekana kuwapinga hii ni sawa kabisa, lakini je hawa mashoga wa kiroho mbona watu hawawapigi marufuku au kuwapinga, mfunguke hawa ni wale wale katika roho ndio sababu imetimia katika mwili wanavaa vitu vya kike, na kama umevaa hauelewi madhara yake, sasa funguka acha ushoga wa kimwili na kiroho, jehanamu inawasubiri, mtubu na kuokoka, acha kuolewa na majini na kwa watumishi hao hawaoi wala kuolewa ni sababu katika ulimwengu wa roho ni wake za majini au waume wa majini.

Zaidi fuatilia makala ya Nabii Hebron usome alichonituma YESU na masomo hakika utapona, sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, uniandike jina langu katika kitabu cha uzima wa milele, sitaki tena kuwa shoga kimwili na kiroho na nyoa aina zote za nywele za ndevu za mapepo zote. Mimi siyo mfuasi wa majini tena katika jina la YESU WA NAZARETI, unibadilishe YESU, unilinde siku zote za maisha yangu. Nashukuru kwa kunifanya nisinyoe tena style za kuzimu. Amen.

Ujumbe huu watumie na wengine kwa njia ya facebook, twitter, google, email usambae kila mahali watu wapone, ubarikiwe. Karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, Arusha, Tanzania.


NABII HEBRON.