Pages

Friday, November 14, 2014

JE UNAZIJUA SIFA ZA NABII WA MWISHO?

BWANA YESU ASIFIWE, yeye ambaye ndie Nabii wa mwisho ambaye alitumwa na MUNGU hapa ulimwenguni, kukomboa ulimwengu, nitaelezea kwa ufupi kuhusu Nabii wa mwisho, katika vipengele viwili. Kwanza katika kifungu cha kwanza katika biblia kuhusu Nabii wa mwisho. Alikuwa ni YESU WA NAZARETI peke yake, na katika kipindi kile na katika kipindi hiki cha mwisho MUNGU ameteuwa mtu ambaye ndio Nabii wake wa mwisho lakini katika sehemu hii watu wengi wanapotoshwa na bado wanazidi kupotoshwa na watumishi ambao wanajiita wao ni Nabii wa mwisho na kumbe ni waongo watupu. Wanamsingizia MUNGU kuwa wao ndio Nabii wa mwisho, hii imetokea katika ulimwengu wote, ni wengi wanaojiita hivyo.

Sasa unatakiwa ujiulize je MUNGU alisema atakuwa na manabii wengi wa mwisho? Jibu, siyo, huu ni uongo na sababu ni baada ya watuishi kumsaliti YESU ikaingia roho nyingine ya kuasi hivyo kujiita yeye ni Nabii wa MUNGU wa mwisho hivyo usishangae, ujue analo pepo, ila nitakufundisha ili upate kupona na umuelewe kimwili yule ambaye ndiye Nabii wa mwisho wa MUNGU, ina maana akiwa yeye ndio Nabii wa kweli wa MUNGU wa mwisho, kwanza MUNGU hatamnyanyua Nabii yeyote yule mwingine sababu MUNGU yeye siyo kigeugeu.

SIFA ZA NABII WA KWELI WA MWISHO ALIYETEULIWA NA MUNGU MWENYEWE…

a.      Nabii huyu hatakufa kimwili wala kiroho atafanya kazi ya YESU aliyotumwa mpaka siku ile ya unyakuo amkabidho YESU watu na ripoti ya kazi aliyoifanya.

b.     Hujua majibu ya viumbe vyote na nchi zote na hakuna jambo lolote ambalo litamshinda yeye sababu  ndani yake yeye ni MUNGU anaishi.


c.      Haabudiwi kama MUNGU au YESU.

d.     Habatizi watu kwa majina yake, wala haibadilishi biblia akaongeza maneno yake.


e.      Siyo mzinzi, muuza madawa, mchawi, freemason, siyo mfanya biashara ya aina yeyote.

f.       Anaongozwa na MUNGU peke yake wala siyo kutumia akili zake.


g.      Unabii anaoutoa unatimia kila anaposema, hanyang’anyi watu mali zao wala pesa zao, na hafanyi kazi ya MUNGU kwa kutafuta pesa kama ilivyo leo hii,wamekuwa ni wezi wanalichafua jina la YESU na MWENYEZI MUNGU.

h.     Endapo Nabii atasema yeye ndio Nabii wa mwisho halafu akafa kimwili sasa upate picha huyo ni muongo kabisa na kama angekuwa yeye ni wa mwisho nikuulize swali je mbona hatujanyakuliwa? Na bado tupo hapa ulimwenguni? Au je sasa tupo tayari katika kipindi cha dhiki kuu? Jibu, bado. Hapo uelewe Nabii wa jinsi hiyo popote katika ulimwengu wote watoto wa MUNGU uelewe huyo anajiita jina hilo na kumkufuru MUNGU na pia kwa picha hiyo hata branch yake itakuwa inao msingi wa uongo na ni mahali pa kuulia roho za wana wa MUNGU.


i.        Siku zote Nabii wa mwisho hawezi kuimaliza kazi aliyotumwa na MUNGU ni mpaka katika siku ya unyakuo, atakapokuja YESU kulinyakua kanisa na yeye ndiye atakayekuwa wa kwanza kushikwa mikono na YESU na kukumbatiwa kwa ajili ya pongezi ya kazi aliyoifanya wala siyo kinyume. Hivyo inapotokea au itatokea hapa mataifa yote mfunguke ufahamu. Shetani amewapa manabii wengi vyeo vya uongo ili kuwapotosha watu ili wawaamini wao ili watu watekwe. Ila umshukuru MUNGU sababu umeelewa sasa ukweli na ujitenge nao na uyachunguze matendo yao, hapa nimeelezea kidogo kwa upande wa kimwili ila kwa upande wa kiroho wewe omba utaijua kweli aliye Nabii wa mwisho na wa kweli.

j.        Kila jambo linatokea liwe zuri au baya iwe ni katika kanisa lake, nchi yake, ni lazima MUNGU amjulishe yeye kwanza na haiwezi ikatokea pasipo yeye kujua, na inapotokea na kuleta madhara kwa watu wake sasa uelewe kabisa huyo siyo, sababu biblia inasema MUNGU hatafanya jambo lolote bila kumjulisha Nabii wake. Sasa iwaje asijue? Jibu unalo.

NOTE:
YESU anachukia sana watu wanaomchafulia MUNGU majina yake ambayo hajawapa, hawajui, ila yeye atapambana nao, neno la MUNGU halirudi bure, maneno haya siyo yangu mimi Hebron, ni maneno yaliyotoka katika serikali ya mbinguni kwa ajili ya mataifa yote.


NABII HEBRON.