Pages

Tuesday, November 18, 2014

JE UNAJUA KILA UNAPOVAA  NGUO ZA MTUMBA UNAJIKABIDHI KUZIMU?
JE UNAJUA NGUO HIZO UNAIVAA MIZIMU YA WENYE HIZI NGUO?
NA JE UNAJUA KUWA UNAPOVAA MTUMBA UNAFUNGULIA MALANGO YA MIZIMU KATIKA MAISHA YAKO?

BWANA YESU ASIFIWE, YESU WA NAZARETI, ambaye ndiye mtoto wa pekee wa MUNGU na ndiye ambaye kupitia jina lake tunapona na unampiga shetani. Katika blog hii nawaelezea kuhusu nguo za mitumba au mavazi ya mitumba, hasara zake, sababu hata mimi sikuelewa hayo ni mpaka pale YESU aliponifundisha mwenyewe sababu hata mimi Hebron nilikuwa nazo nyingi sana ila aliponijulisha mara moja nilizichoma siku bakiza hata moja. YESU akanieleza Hebron ningemtuma nani? Sasa uyajue haya na watu wapone, ila nimekujulisha wewe uliyenikubali ili niuokoe ulimwengu kupitia mwili wako, akaniambia Hebron nilikueleza nitautumia mwili wako kuukomboa ulimwengu huu lakini huu mwili wako ni mtakatifu sababu mimi ninaishi ndani yako ila usiogope sababu ya haya ninayokueleza. Hizi nguo za mtumba unapozivaa huwa unanajisika ndani yako, niliogopa sana, ni sababu ya nguo hizo, zina mizimu na mapepo na ni mali zao.

MTUMBA NI NINI?

Mtumba ni kitu chochote ambacho kimeshamilikiwa na mtu wa kwanza likiwa kipya nay eye, na linapotumika na mtu mwingine yeye anakuwa anatumia mabaki ya mtu mwingine.

MADHARA YAA KUVAA MITUMBA.

Unapokuwa unavaa nguo ya mtumba au viatu au mkanda au nguo yeyote ile, ile nguo inakuwa inayo mizimu ya hao watu ambao ndio waliokuwa wamezivaa kwanza. Na unapovaa mtumba uelewe kuwa kama yule mwenye nguo alikuwa na mikosi na wewe utaipata tu sababu umeivaa nguo yake ndio sababu inaitwa mtumba, kama alikuwa anayo madhaifu ya aina yeyote ile na wewe utayarithi, iwe ni magonjwa, tabia za ajabu, uzinzi, ulevi, hasira, uwizi, uongo, ni mchawi, ni freemason, unapovaa na wewe hiyo mizimu inakufuata ulipo sababu ya hiyo nguo yao ambayo wewe umeivaa.

Najua mitumba imetoka katika mataifa mbali mbali na nchi nyingi raia wake wanavaa nguo za mitumba, ila hawaelewi madhara yake ni nini kiroho. Mimi aniponifunulia haya YESU WA NAZARETI ni sababu ananipenda, na mimi nawafunulia ulimwengu wote ni sababu YESU wa mataifa yote anawapenda na anataka mpone ili awabariki na awaokoe na shetani asipate kitu cha kukushtaki na shetani asipate chochote cha kukuibia.

Nataka uelewe jambo hili, je utakuwa unajua nguo za mitumba unazovaa ni za mtu aliyekufaga au yupo hai? Jibu haujui. Na je unajua kuwa katika kila nguo ya mtu kuna vitu vyake vinakaa hapo? Tazama vazi la Eliya lilikuwa lina vitu vya Eliya na alivyolipokea Elisha nay eye akavipokea, hivi ndivyo ilivyo nguo zote za mitumba inavyo vitu vya watu na unapovaa ile mizimu ya kwao inakufuata na kuharibu maisha yako katika roho na kumfanya mtu kuwa na tabia za ajabu ajabu ni sababu ya nguo za mtumba, na cha ajabu hata kanisa linapigwa upofu halikuelewa madhara ya mitumba na kulifanya kanisa ndio msambazaji maarufu wa mitumba ili kuwaletea watu maangamizi.

Ile mizimu ya yule ambaye umevaa nguo yake inakuwa inakuja kukumiliki wewe katika maisha yako kiroho na kimwili na ndio sababu utakuta watu wanampenda MUNGU lakini hawaokoki hii ni sababu mizimu wa mtumba unakushikilia na kukutumikisha pasipo wewe kujua. Nguo hizi hazikomboleki.

Kama mwenye nguo hiyo amekufa na yupo kuzimu na wewe unayavaa mtumba  huo utavutwa kuzimu usiende mbinguni, hii ni sababu unalo vazi lake yeye aliyekuwa mmiliki wa vazi la kwanza.

Kama mwenye nguo wa kwanza yeye ni freemason na wewe unayo vazi lake, kule kuzimu mizimu inakuona wewe ni mtu wao na itakufuatilia inahakikisha tu na wewe unamfuata mwenye nguo hiyo.

Unapovaa mtumba uelewe mlango wa shetani kukupata upo wazi kabisa na mapepo kukuvamia, hata kama unalalia mashuka, blanketi za mitumba kila unapolala na wewe unachukuliwa nafsi yako unapelekwa kutumikishwa kama msukule na siku zote maisha yako ni shida na mahangaiko tu.

Kila ukivaa mtumba uelewe umevaa mizimu, sasa watu wengi hawapendi mizimu wanaipiga ila wameivaa, hapo umejisumbua, jibu ni kuacha kuvaa mitumba upone, ili Baraka zako zikae katika hekalu la MUNGU ambalo ndio mwili.

Nguo za kurithishwa za watu wallliokufa hizo pia ni mtumba, zinazo madahara makubwa sana. Unayavaa madhaifu ya aliykufa na hata kujiunganisha na kifo alichokufa, kama amekufa cha HIV na wewe itakufuata au ajali au ugonjwa fulani na wewe linakufuata, au kama marehemu alikuwa na matatizo na wewe unayarithi. Jambo hili ni hatari kweli. Je ni salama kwa picha hii uliyoipata? Mimi Nabii Hebron ninajua shetani hanipendi kabisa na ukweli hata mimi simpendi. Zaidi ya 100% na kupitia blog hii na mafunuo ninayowaeleza watu wote wa mataifa yote, sasa hivi shetani anatoa machozi hapa ninapoandika ujumbe huu ninamuona analia machozi ila sina huruma kwa shetani, analia anasema Hebron usitume somo hilo sababu sitawapata watu niwachezee maisha yao na kuishi katika miili yao.

Nitaelezea kuhusu nguo za ndani za mtumba. Kila unapovaa nguo ya mtumba ya ndani, kile kiungo chako cha siri linakuwa ni cha mizimu na mizimu wanakuoa au kukufanya mume wao na kukuwekea tabia za uzinzi, utajitahidi uache lakini unashindwa ni sababu ya hiyo nguo ya ndani ya mtumba, na ndoa zinaharibikia, na pia mapepo hupitia katika njia hiyo kuharibu uzazi, au kumfanya mwanamke atoke damu kupitiliza siku. Mizimu ndio inayofanya hayo, inakunywa damu yako ni chakula chao ila wewe binadamu haujui.

NOTE:
Kuvaliana nguo pia ni hatari kiafya na kiroho. Kiafya kama mtu anayomagonjwa ya mwili na wewe utayapata na kiroho mtu anapovaa nguo yako anavaa na matatizo yako, balaa, mikosi, magonjwa ya kurithi, kama ni masikini na wewe unauvaa, mlevi na wewe unauvaa, muongo na wewe unauvaa uongo. Kwa njia hii wengi zaidi shetani amewateka, ashukuriwe YESU pamoja na serikali yake ya mbinguni akiwamo Eliya, Musa, Ibrahim wa mbinguni wanaonifundisha na wote 24, MUNGU awabariki sana.

Unapovaa mtumba kama aliyevaa mara ya kwanza katika ukoo wao hawafanikiwi na wewe inakufuata hivyo hivyo.
Unapovaa mtumba ROHO MTAKATIFU haishi ndani yako sababu unakuwa umelifunika hekalu lako.

Unapovaa mtumba ile mizimu inakuja kukuibia vitu vyako mfano Baraka zako ulizokuwaga nazo umepewa na MUNGU, na kukutesa.

Na unakuwa hata kama umeokooka shetani alikukosa au amekutafuta katika ulimwengu wa roho hakuoni. Ila endapo ukiwa umevaa mtumba tu tayari anakuona ulipo sababu ile nguo uliyovaa inakuwa na mizimu, na mizimu inayo uhusiano mkubwa na shetani.

Viatu vya mtumba, viatu hivi unapoivaa kama nilivyoelezea kuwa siku zote katika kitu cha kuvaliwa na mtu wa kwanza ni chake tu, hivyo hivyo mizimu inabakia katika viatu hivyo unavyozivaa tu, hivyo mizimu inaiba utayari wa maisha yako, utayari wa kuokoka, kwenda mbinguni, utayari wa mafanikio yako katika maisha yako na ndio sababu hata kimwili fuatilia utaona watu wengi sana wanaovaa mitumba wachunguze au kama ni wewe jichunguze. Matatizo hayaishi na unafanikiwa kwa shida au hata haufanikiwi, hii ni sababu siku zote aliyekufa ambaye ndiye mzimu hupendi ufanikiwe huku ulimwenguni ni hivyo atahakikisha tu na wewe usifanikiwe. Inawezekana aliyekufa yeye hajaolewa au hakuoa na wewe atahakikisha na wewe hufanikiwi katika eneo hilo au yeye hajasoma na wewe hautasoma, au yeye  hakuwa tajiri atahakikisha na wewe unakuwa maskini tum au yeye alikuwa ni mchawi, freemason, tapeli atahakikisha na wewe yanatokea kwako.

Jambo lingine mitumba kama nilivyoelezea madhara yake kiroho katika mitumba ni mkusanyiko wa nguo za watu wengi idadi hakuna ajuaye. Sasa inamaana pia inakuja na maroho ya mizimu ya mataifa mbali mbali na madhaifu mbali mbali na unapoivaa na wewe unakuwa unayakaribisha katika mwili wako.

Unakuwa kama mtu asiye na msimamo kiroho na kimwili na hatima yako labda neema ya MUNGU ikushukie vinginevyo siku unakata roho wanakuchukua wanakupeleka kuzimu sababu wanao uhalali na wewe.

NOTE:
Ili maisha yako isiwe na balaa epuka mitumba, na usivae hata kurithishwa nguo za watu waliokufa tayari hiyo inakuwa ni mtumba. Watu wengine wanasema itakuwaje nitavaa nini. Yakupasa kumshukuru YESU ambaye amenifunulia mimi Nabii Hebron wa kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, ili ugonjwa huu sugu uliyofichika sasa unafichuliwa ili watu wapone roho zenu.

Roho za mfilisi zimeambatana na biashara ya mtumba, omba MUNGU akupe biashara ya nguo mpya. Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote. Uniokoe, uniandike katika kitabu chako cha uzima wa milele.  Na univue mavazi ya mitumba na mizimu iachie maisha yangu ili unimiliki wewe. Nifungulie milango ya nguo mpya na mimi nivae mpya. Amen.


NABII HEBRON.