Pages

Thursday, October 16, 2014


PEPO BENEDICT NI PEPO GANI?

NDIYE PEPO ALIYEANZISHA UBATIZO WA KIKOMBE NA NYINGINEZO!

BWANA YESU ASIFIWE, katika somo hili nitaelezea kuhusu pepo linaloitwa Benedict. Huyu ni pepo moja wapo mkubwa na yeye alikuwepo kuzimu ila kwa sasa nimeshamuangamiza kabisa pamoja na kazi zake ambazo alikuwa anazifanya kwa ajili ya kuwapotosha wanadamu wasimfuate YESU wa kweli bali wamfuate yesu wa uongo. Pepo huyu ndiye aliyeanzisha ubatizo tofauti na ule wa YESU wa Yordani na ule ubatizo wa Yohana, ubatizo ambao ulitoka kwa MUNGU ili watu waoshwe dhambi zao zote. Sasa pepo Benedict katika kitengo chake cha kanisa la shetani, na yesu wa uongo wakabuni mbinu za kuwateka wanadamu ili wasije wakaoshwa dhambi zao na YESU wa kweli, wakabadilisha ubatizo tofauti na formula za biblia ya MUNGU wa kweli. Na ndio sababu katika dunia hii utaona watu wanabatizwa ubatizo tofauti na YESU uelewe hao hawajaoshwa dhambi zao mpaka sasa na pia siyo mwili mmoja na YESU wa kweli, sababu kubwa ni njia ya ubatizo wa uongo ambao haupo hata katika biblia ya kweli ila upo katika biblia ya shetani, mimi nimeiona na najua kilichoandikwa ndani yake. Na ndio sababu nawaeleza ukweli ili mpone jamani.

Pepo Benedict ndiye aliyebuni ubatizo wa kikombe, ubatizo wa watoto wadogo, ubatizo wa kisima, ubatizo wa maji mengi ila mtumishi anakubatiza kwa jina lake. Hii yote ni ili wewe utekwe na upigwe upofu uone upo salama kumbe umeshatekwa. Batizo hizi zote asili yake ni kuzimu na siyo mbinguni, sasa ujiulize je kuzimu inaokoa? Kuzimu kuna YESU wa kweli? Kuzimu inatoa msamaha wa dhambi? Jibu unalo. Huyu pepo ndiye aliyebuni ubarikio wa watu wazima. Niwaulize je mpo tayari kufuata yaliyomo katika biblia ya YESU wa kweli au wa uongo? Ukifuata ya uongo tayari na wewe unakuwa ni mtoto wa yesu wa uongo. Mimi Hebron alipokuwa ananifundisha YESU ili niifanye kazi yake na aliponieleza Hebron sina watu ninao wachache sina, wengi ni wa shetani, niliogopa, akanieleza mengi ambayo ni yangu binafsi na alivyosalitiwa na mahali wanapochukua masomo ya chuo cha kuzimu ambacho jina la chuo hicho cha elimu ya uongo, principal wake anaitwa AMAKUTA. Huyu na yeye nimemuangamiza, huyu ni jinni mwalimu wa uongo. Sasa ubatizo wa uongo, kuabudu sanamu, vyote vilikuwa vinatengenezwa na jinni Amakuta halafu wanaleta duniani na watu mnapokea injili ya uongo, mnakufa roho zenu na hamuendi mbinguni. Sasa unafunguka ufahamu. Tafuta katika biblia, ukiona ulibatizwa tofauti na YESU ujue umepokea ubatizo wa pepo Benedict, na hiyo ndiyo dalili ya kuwa wewe siyo mkristo wa kweli. Ni sababu ubatizo wako siyo wa neno la kweli kutoka katika biblia unayoijua bali ni ubatizo uliopo katika biblia usiyoijua. Je hauoni umepotea, mshukuru YESU ambaye amenifunulia haya ili upofu wa kiroho ukutoke na sasa uone nuru ya kweli.

Uokoke sasa BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote uniokoe, uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima, uniondolee ubatizo wa pepo Benedict, uniongoze nikabatizwe ubatizo wa kweli ambao ulibatizwa wewe YESU WA NAZARETI. Amen.


NABII HEBRON.