Pages

Saturday, March 14, 2015

JE UNAJUA KUWA UKIBATIZWA UBATIZO TOFAUTI NA ALIOBATIZWA YESU UNAKUWA UMEBATIZWA NA PEPO LINALOITWA HIDAN?
SOMA HAPA….

Nawasalimu kwa jina la YESU WA NAZARETI aliye hai na ndiye aliye mwana wa pekee wa MUNGU. Napenda kuwajulisha mataifa yote mnaompenda YESU na YESU anawapenda nyie sana, ila shetani anawaonea wivu wanadamu sababu anajua wataenda mbinguni siku moja mahali palipo pazuri sana alipofukuzwa yeye lusifa, na baada ya hapo MUNGU akatengeneza njia ya agano la ubatizo wa maji mengi yanayotembea kama Yohana mbatizaji alivyoonyehsa njia na YESU na yeye akabatizwa ili kutuonyesha njia, na sisi wote ili tuwe na agano na MUNGU ni lazima tuokoke na kubatizwa kama yeye. Ila sasa pia mpango huu ambao MUNGU aliuanisha ili kuweka agano na wanadamu kwa njia ya ubatizo wa maji mengi kwa sasa shetani amefanikiwa kulizuia hili agano la ubatizo wa maji mengi ili wanadamu wasiwe ni wakristo wa kweli, wasiende mbinguni, na wasiwe wana wa MUNGU bali wabakie wana wa shetani, hata wanadamu wasijielewe wametekwa na shetani.

Ila nawafunulia siri hii ili mpone sababu hata mimi Hebron sikuyajua haya na nilifikiri nipo salama kumbe nilishatekwagwa. Ila neema ya MUNGU iliniokoa na hata sasa MUNGU bado neema yake ipo hivyo, uchukue hatua leo uokoke na ukabatizwe ubatizo wa maji mengi ambao upo katika biblia na unajulikana na MUNGU. Sasa hizo batizo nyingine zote mfano ubatizo wa maji ya kikombe, ubatizo wa maji ya kisima, kubatizwa kwa maji mengi kwa jina la kiongozi wa dini au pastor au kwa jina la mtu yeyote yule, uelewe wewe umebatizwa na pepo kiongozi anayeitwa HIDANI, yeye huyu ndiye aliyetumwa na joka kuu kueneza aina hizi za batizo kwa wakristo ili wasiingie katika agano na YESU bali waingie agano na shetani, haijalishi limetajwa jina la baba, mwana na roho mtakatifu au la YESU.

Nataka uelewe kuzimu yupo mungu wao anayeitwa joka kuu, yupo mwana wa pekee ambaye ndiye shetani, yupo roho mchafu ambaye anaitwa Maxwell. Hawa wote ndio wanaoingia agano na hao wote ambao wanabatiza ubatizo ambao haujatokea mbinguni bali ubatizo wa akili zao. Hii yote ni ili kuwapoteza wanadamu wajione ni wakristo na wamekamilisha ahadi za kuwa wana wa MUNGU. Kumbe mpaka sasa ni wana wa shetani hata ukristo wa jinsi hii ni ukristo wenye agano la shetani, sababu tafuta katika biblia hakuna aina za ubatizo hizo. Na ukisoma katika kitabu cha Ufunuo 22:18-19; ole wake aongezaye neno la MUNGU au kulipunguza. Sasa hauoni hapa hii laana inamhusu kila aliyebatizwa na kubatiza tofauti na biblia ina maana yeye ni adui wa YESU na kama ni adui wa YESU basi yeye ni rafiki wa shetani. Zaidi ingia katika www.prophethebron.org; ingia katika link ya blog, soma kitabu cha ubatizo wa kweli kwa ulimwengu wote kilichoandikwa na Nabii Hebron utafunguka zaidi na utajua ni wapi ulitekwa, na wewe ni rafiki wa YESU au rafiki wa shetani.

Najua hampendi urafiki na shetani, sasa utii ubatizwe kama alivyobatizwa YESU uingie agano na yeye. Usikubali hata familia, rafiki zako na wengineo wabatizwe ubatizo ambao unawafanya wawe adui na YESU na kuwafanya watu wasiwe wakristo wa kweli bali ni wakristo waliopoteza direction ya mbinguni kwa kuingia agano la pepo Hidani. Pepo huyu hukaa katika vichwa vya kila mtu aliyebatizwa ubatizo tofauti na YESU, yeye hukaa katika paji la uso wa watu kama ni alama huyu ni wa shetani. Hivyo katika ulimwengu wa roho unaonekana mtu wewe ni wa shetani na umesaini hilo agano ulipobatizwa. Ili upone ubatizwe upya hiyo saini ifutike na usiabudu katika mahali wanapobatiza watu tofauti na biblia ilivyoagiza na pia utakaposhiriki tu uelewe utanajisika tena sababu hizo madhabahu ni za miungu ya dunia hii hapo hayupo MUNGU wa mbinguni

Sasa rejea ili upone, uwe mkristo mwenye agano na MUNGU wa mbinguni badala ya agano la miungu ukabatizwa ubatizo wa miungu, ukasali katika ibada za miungu pasipokujua, ukijua wewe ni mkristo kumbe ni mkristo mfuasi wa mpinga kristo. Moja ya sababu itakayo kuhakikishia wewe ni mpinga kristo bila kubisha. Nikuulize swali, mbona umebatizwa ubatizo tofauti na YESU? Kivipi hivi? YESU alibatizwa akiwa mtu mzima, wewe umebatizwa ukiwa mtoto mdogo. YESU hakuwa na mama wa ubatizo wala baba wa ubatizo, alienda peke yake, ila wewe ulienda nao. YESU aliokoka kwanza, wewe haujaokoka mpaka sasa. YESU alibatizwa katika maji yatembeayo, wewe umebatizwa katika maji ya kisima. YESU alibatizwa kwa jina la BABA, MWANA, NA ROHO MTAKATIFU, wewe umeongezewa na jina la mchungaji. YESU alizamishwa kwenye maji mengi mwili wote, wewe umedanganywa na hao waongo wakakumwagia maji  matone kichwani.

Ndugu msomaji wa makala ya Nabii Hebron mpaka sasa somo umelielewa na wewe uwatumie na wengine makala hii na watapona na utabarikiwa sababu watu wataenda mbinguni na kugombana na shetani. Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, niliingia agano la ubatizo wa shetani pasipokujua au kwa kujua, naomba uniongoze kwa mtumishi unayemtumia wewe anibatize niingie agano na wewe nifute saini zote za pepo Hidani. Akae katika paji langu la uso Roho wako mtakatifu tu kama alama yako ujue mimi ni wako. Amen.

Zaidi ikishindikana karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, utabatizwa na uingie agano na YESU, uwe mkristo na rafiki wa YESU sana.


NABII HEBRON.