Pages

Friday, January 2, 2015

MAHUBIRI YA NABII HEBRON KUPITIA REDIO KUHUSU UBATIZO WA KWELI 2012.
Asante sana ndugu mtangazaji. MUNGU akubariki
Kwanza kabisa nitaomba kwa ajili ya wasikilizaji wote wa kipindi hiki,

BABA yangu na MUNGU wangu uketie mahali pa juu, nina libariki jina lako nakulitukuza, nakuinua juu sana, sana. Maana hakuna kama wewe, wengine wote ni wa uongo, wewe ni MUNGU uliye hai, uliyeumba ulimwengu mzima, hata huyu anayekusikiliza ni wewe umemuumba, pia mimi. BABA yangu asante, ninawafungua wasikilizaji wako, natuma Malaika fahamu zao, akili zao. Nina ondoa pamba kwenye masikio, nguvu zote za upinzani ndani yao, ili wasisikilize  hili jambo ambalo unaenda kuwafundisha watoto wako lisiingie, lazima liingie kwa nguvu na mamlaka ya jina lako ulilonipa, maana wewe ni MUNGU. Ukisema umesema, maana sasa ni wakati wa kila mtu kujua ukweli ili wasiangamie, wewe ni kweli, na wewe unawapenda.

BABA yangu Asante, sifa na utukufu na kurudishia wewe, asante kwa muda huu

Asante kwa Malaika wako walioshuka mahali hapa kuyashuhudia haya sasa hivi akiwepo Malaika Gabriel.

Asante naomba uzidi kuwabariki sana.

Ndugu msikilizaji leo nina mambo ambayo nitaelezea kwa undani zaidi ambayo ameniagiza Bwana YESU ambaye ndie njia na uzima na kweli zaidi, tunayemuabudu na tunayemsubiri,

Katika mambo nitakayozungumzia zaidi ni kuhusu Ubatizo ni nini? Kwanza
Jambo la pili ubatizo wa kweli ni nini?
Jambo la Tatu, faida ya ubatizo wa kweli
Jambo la Nne: hasara za kubatizwa kinyume na mpango wa MUNGU
Jambo la Tano: jinsi MUNGU anavyotaka ubatizo ufuatwe na ubatizo ambao ni mapenzi yake yeye mwenyewe alioanzisha mbinguni.
Jambo la Sita: mambo yanayokwenda kutokea Tanzania.

BWANA YESU ASIFIWE sana,
Ndugu msikilizaji MUNGU akubariki mahali ulipo.

Nitaanza kuhusu ubatizo, ubatizo ni kiapo kati ya mwanadamu na MUNGU aliye hai, aliyekuumba na aliyeumba ulimwengu pamoja na wewe  ndugu msikilizaji, ubatizo ni agano lako kati yako wewe na MUNGU ya kwamba wewe ni wake wala si wa mwanadamu au kitu chochote au dini.

Ubatizo chanzo chake ni MUNGU mwenyewe, ndiye aliyepanga akiwa na maana nzuri na nia njema kwa ajili ya mwanadamu aliyemuumba kwa faida yake yeye mwenyewe MUNGU.

Na sababu nyingine ya MUNGU kumuumba mwanadamu, amemuumba ili amuabudu yeye tu na sio kitu kingine chochote sababu nyingine atawale kila kitu, maana hivi viumbe vyote aliviumba ili mwanadamu avitawale.

Ukisoma katika kitabu cha  Mwanzo 1:26, baada ya anguko la mwanadamu, shetani  akavuruga ulimwengu na akijua ya kwamba ndiyo ameshinda na atatawala ulimwengu, na wana wa adamu wote, baada ya haya kukatokea ndipo MUNGU akaanzisha huduma ya ubatizo ili kuwasafisha na kuwakomboa wanadamu kupitia maji, kwanza kabisa MUNGU alimtuma Yohana aje ulimwenguni kuja kubatiza, Yohana ni mnadhiri wa MUNGU aliyetoka mbinguni , akiwa mbinguni alitumwa na BABA kuja kumtengenezea njia yaani YESU, ukisoma katika kitabu cha Yohana 1:15-18 inaelezea kabla ya ujio wa YESU.
Yohana nabii alitabiri. Na juu ya nabii isaya pia alitabiri ikatokea. Yohana akazaliwa na Elizabeth na YESU ilitabiriwa hivyo hivyo ikatokea, hawa wote ukiangalia jinsi wazazi wao walivyopata ujauzito ni kwa njia ya ROHO MTAKATIFU, hata ukisoma kitabu cha Mathayo 1:18-28 Luka 11:38 inaeleza vizuri kabisa au kwa njia ya mpango MUNGU mwenyewe wake ili kuukomboa ulimwengu huu. Yohana akazaliwa na akatenda yale yote aliyoagizwa na MUNGU. Aje ulimwenguni afanye  yale yote alioagizwa na akabatiza sawa sawa na  MUNGU, huku  ulimwenguni  na alifanya na alibatiza sawa sawa alivyoelezwa na MUNGU,  Ukisoma  Mathayo 3:11; Yohana alibatiza kwa maji mengi ikiwa ina maana  kusafisha.

BWANA YESU asifiwe
Ndugu msikilizaji natumaini mpaka sasa umeelewa Ubatizo ni nini, na chanzo chake ya kuwa ni MUNGU mwenyewe ndiye mwanzilishi na wakati Yohana akibatiza na yeye alikuwa akieleza habari ya YESU, yakuwa yeye ni mkuu sana hata yeye Yohana alikiri sistahili kufunga kamba za viatu vyake.

Ndugu mskilizaji  hapa hata Yohana aliyetoka mbinguni akatumwa ulimwenguni anakiri YESU ni mfalme na yeye alibatiza kwa Roho na Moto, ukisoma katibu  cha Mathayo 3:11 na hata Yohana aliogopa kumbatiza YESU kwa ajili  ya ukuu wake alionao, lakini YESU alimwambia Yohana kubali hivi sasa kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote, basi akakubali na YESU alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini, na tazama mbingu zikamfungukia akaona Roho wa MUNGU akishuka kama Ua, akija juu yake na tazama sauti kutoka mbinguni ikasema huyu ndiye mwanangu mpendwa wangu niliyependezwa nae, imeandikwa katika kitabu cha Mathayo 3:15-17 soma.

Ndugu msikilizaji Mtoto wa MUNGU tena unafanana yeye, MUNGU azidi kukuinua na kukufungua ufahamu wako zaidi uelewe haya ninayokueleza MUNGU akutengeneze zaidi na akusikilize. Na MUNGU azidi kukufungua ufahamu wako ili uelewe zaidi kuhusu ubatizo alioagiza MUNGU, watu wote wabatizwe. Ukisoma katika injili ya ubatizo wa Yohana utaona alifanya yote aliyoagizwa na MUNGU ili tu ukombolewe maana pasipo kubatizwa hauendi Mbinguni. Ukisoma katika kitabu cha Yohana 3:5-7 inaelezea vizuri bila kubatizwa hauendi mbinguni, YESU alibatizwa kwa maji mengi, kwa maana ndivyo ilivyoagizwa na akafanya kama yeye alivyotaka kufanya, na YESU alikuja ulimwenguni ili kuukomboa na kwa sababu alikuja ulimwenguni, kwa njia ubatizo ilimbidi na yeye abatizwe  kupitia ubatizo aliobatizwa.
Na sisi sote tubatizwe kama yeye ambaye ndiye tunaye mwamini na ni ndiye njia na uzima na kweli soma katika kitabu cha Yohana 14:16 kama YESU ndiye njia ya uzima na kweli inabidi tufuate yale yote aliyoagiza, ndio njia ya kutupeleka sisi mahali alipo, na MUNGU alimtuma Yohana kubatiza, hakusema awe na msimamizi mwanadamu, msimamizi wako ubatizo ni ROHO MTAKATIFU.

Halleluya, inatia huruma sana yaani utaona baada na hata kabla ya YESU kubatizwa hakukuwa na msimamizi mwanadamu msaidizi, msimamizi.

Sasa mpaka hapa natumaini umezidi kuelewa kuwa katika Ubatizo siyo mwanadamu msimamizi, ni ROHO MTAKATIFU na siyo mwanadamu, angalia mfano YESU alivyobatizwa na Yohana na mpaka YESU alivyobatizwa.  Na pia na wale mitume wa YESU, walivyo batizwa, nao walivyowabatiza watu, bila wanadamu wasimamizi. Walivyobatizwa walisimamiwa na ROHO MTAKATIFU tu, na ndio mpango wa MUNGU, na ubatizo unasimamiwa na ROHO MTAKATIFU na siyo mwanadamu.

Lakini siku hizi agizo aliloagiza MUNGU limeachwa, madhamini wako wa ubatizo ni mwanadamu tena lazima awe mwanamke au mwanaume, huo sio mpango wa YESU ni mpango wa shetani, ili kuangamiza watu wasiende mbinguni. Ameniambia YESU, waambie ulimwengu mzima hashiriki huo ubatizo feki narudia tena, ubatizo huo ni feki haujatoka kwake, hajalishi wanamtaja jina lake, baada ya ubatizo YESU alishukiwa na Ua ili kumshuhudia huyu ni mwana wa MUNGU na baada ya kushukiwa ROHO MTAKATIFU hapo ndipo YESU alipoanza kuongozwa na ROHO MTAKATIFU na huyo mdhamini ambaye anayeushirika na MUNGU asilimia mia 100%  akamuongoza kuyashuhudia matendo ya MUNGU, kumtia nguvu mwana wa MUNGU. Hivi ndiyo inavyotakiwa katika ubatizo, ROHO MTAKATIFU tu, siyo mtu asimamiwe na mtu.

Halleluya! BWANA YESU ASIFIWE,

Upate kufunguka na watu wajue ukweli maana katika neno lake wa kwanza atakuwa wa mwisho, na wa mwisho atakuwa wa kwanza. Haya yote yalianza kwa watu weupe nao wamepuuza, lakini sasa tokea Africa na Tanzania Nchi yako. Itajulikana, watu wamjue MUNGU.

BWANA YESU ASIFIWE!

Ndugu msikilizaji naomba uendelee kusikiliza ni kwa faida yako wewe, halleluya!

Mwana wa MUNGU hivi ndivyo inavyotakiwa katika Ubatizo ni ROHO MTAKATIFU tu, siyo mtu anayesimamia.

Haya ni mapokeo ya mwanadamu ambao baada ya YESU kupaa mbinguni shetani akawaingia wale ambao, hawakumtii ROHO MTAKATIFU na kubadilisha mpango wa MUNGU katika Ubatizo, na walibadili ubatizo wa maji mengi, baadhi yao wakaanza kubatiza kwa kutumia beseni au kikombe, kubatiza tena vitone vya maji kichwani tu, nikuulize, Je wewe msikilizaji, je Yohana ndiye aliyebatiza hivyo? jibu hapana.

Ndugu msikilizaji MUNGU akutie nguvu akuinue na upate kuelewa ukweli, na kama jibu ni hapana na kwa MUNGU ni hapana. Yohana hakufanya hivyo na hata mbinguni ubatizo huo haupo na kama haupo mbinguni, huo ubatizo umetoka wapi? Jibu hapana kwa shetani

Haijalishi wana litaja jina la YESU, huo ni ubatizo feki, ameniambia YESU niwaeleze ulimwengu wote, ikiwa ina maana mataifa yote, watu wote, mabara yote, bila mipaka, makabila yote wamjue YESU.

Jina lake linatumiwa vibaya watoto wake wanaangamia kwa ajili ya watu wanaobadilisha mpango wake MUNGU, akasema mwanangu Hebron watoto wangu wananipenda sana ila hawaambiwi ukweli kuhusu mimi  98% shetani ameliteka kanisa ulimwengu wote imebakia asilimia 2%  tu ndiyo inajua, ndio sasa waeleze watabizwe ubatizo niliobatizwa mimi YESU, watu wanajua kwamba mimi ni njia na uzima na kweli, na hakuna atakaye fika kwa Baba pasipo mimi YESU.

Mimi YESU nilikuja ulimwengu ili nionyeshe njia ya kwenda kwa Baba yangu hakuwa mjinga kuagiza ubatizo wa maji mengi yaani MUNGU hakuwa mjinga kumwambia Yohana mtu akibatizwa asiwepo msimamizi, leo hii nafasi ya ROHO MTAKATIFU imechukuliwa na mwanadamu.

Matokeo yake ni ubatizo batili, nakuuliza wewe unayempenda YESU, Je YESU alivyobatizwa alikuwa na mdhamini.

Jibu ni hapana hivi ndivyo inavyotakiwa mdhamini wako ni ROHO MTAKATIFU na ndiye atakaye kuongoza na kukuombea maishani mwako na  kukupeleka mbinguni nakuuliza swali, Ndugu msikilizaji ili uzidi kufunguka ufahamu wako Je mwanadamu atakuongoza wewe ufike mbinguni? Jibu hapana.  Oohoo…MUNGU tusaidie.

ROHO MTAKATIFU ndiye atakayekusaidia kufika mbinguni na kukushindia hapa ulimwenguni. Kama YESU alivyoshinda. MUNGU tusaidie kweli yako imeondoka, MUNGU kuwa mjinga kutupa ROHO MTAKATIFU au mdhaimini katika ubatizo wake, yeye alijua kwamba ROHO MTAKATIFU ana umoja na wewe au kwa Lugha nyingine rahisi ili uelewe ROHO MTAKATIFU ni mojawapo ya nafsi ya MUNGU wajue kwamba zote zina umoja, BABA, MWANA na ROHO MTAKATIFU lilekusudi na kiapo cha ubatizo walipanga wote hawa watatu ili kukupata wewe sasa na kuuliza swali kama wewe haujadhaminiwa na ROHO MTAKATIFU utakwenda wapi? Jibu jehanamu badilika ubatizwe kama YESU alivyobatizwa yeye ndiye njia ya uzima na kweli, njia yake uifuate hakika hautapona Yohana 4:6 inasema usifuate mapokeo ya dini. Fuata muongozo wa ubatizo ulioandikwa kwenye biblia, kitabu kitakatifu cha MUNGU.
Safari yetu ya mbinguni na maelekezo ya mbinguni yameandikwa ndani ya kitabu cha Ufunuo wa Yohana 22:18-19 ameonya ole wake atakaye ongeza au kupunguza kitabu hiki cha unabii sehemu yake itaondolewa katika ule mji mtakatifu, sasa ndugu msikilizaji embu chunguza kwenye biblia kuanzia mwanzo mpaka sura ya kwanza mpaka mwisho nakuhakikishia 100% hakika hautakuta ubatizo wa kikombe yaani wa kichwani. Pili hamna mdhamini katika ubatizo, mwanadamu iwe mwanamke au mwanaume, wote mliofanya hivyo ni mapokeo, haujatoka kwa MUNGU,na kama haujatoka kwa MUNGU na basi umebatizwa ubatizo wa shetani, na wewe umeingia agano na shetani. Sasa hapo utaona kabisa ubatizo umeongezewa mambo mengi na huu mpango wa shetani alioupanga ili wewe usiende mbinguni maana tayari umeenda tofauti na yeye MUNGU lakini wewe hauna shida, shida waliokubatiza na hao waliomsaliti MUNGU na neno lake, ndio wamekuwa vipofu maana hayapo kwa MUNGU. Ni kuulize swali Je MUNGU ni mjinga aliposema kila mtu abatizwe kwenye kijito cha utakaso na azamishwe mwili wote, Jibu ni hapana na Je embu fikiria ufunguke ufahamu wako uwe huru, Je kwa nini ni kichwa tu kinamwagiwa maji tena matone tu, Je MUNGU aliagiza hivyo kichwa kimwagiwe maji Jibu hapana, aliagiza mwili mzima uzamishwe kwenye maji kama YESU alivyofanya. Kama wewe ni mkristo kweli na unafuata ukweli ambaye ni YESU, tunamwamini tumfuate mahali alipo Je hicho kichwa yeye alizamisha kwenye maji? Jibu hapana.

BWANA YESU ASIFIWE.
Ooh MUNGU tusaidie
Ubatizo wa kuzama kwenye maji kama Yohana mbatizaji umetimia na Je huu mwili umeingia kwenye maji wote Jibu ni kichwa tu, kimemwagiwa maji.

Sasa ujumbe ameniambia YESU akanifundisha ukweli niliogopa sana baada ya kujua ukweli maana mimi nilibatizwa hivyo, akaniambia ameshasema na baadhi ya watumishi wangu waseme ukweli na waambie mataifa yote wamenisaliti hawataki kusema ukweli baadhi, wananitaja kwa maji tu midomoni mwao baadhi yao wanafiki.

Lakini ole wao mwisho wao umefika na sasa ni wakati wangu baadhi yao hawasemi.

Mimi nataka mwili wako tu kama nilivyomtumia Paulo, lazima watu wanirudie mimi kazi yake imeanza YESU mwenyewe tangu APRIL 2012 dunia nzima na njia ya kuzimu zote amenipa maelekezo namna ya kufunga kwa hilo walikuwa wanategemea kuchukuwa nguvu hawana pia hawazipati tena, sasa hivi masalia zimebaki baki vinaishia na wataporomoka mpaka ziro hasa watumishi wanaotumia nguvu za giza hii ni kwa ulimwengu mzima tayari na wanajua mambo hayaendi. Nchi zote mabara yote tayari wanajua mambo hayaendi.

Ndugu msikilizaji naomba sasa ujue ubatizo wa kweli. Ubatizo wa kweli ambao MUNGU anaoutaka aliuandaa kwa ajili ya wewe upone akishirikiana na ROHO MTAKATIFU. Mwana wa MUNGU ubatizo wa kweli ndio aliagiza MUNGU ufuatwe, ni ubatizo aliobatiza Yohana, ni ubatizo aliobatizwa YESU tu huo ndio ambao upo kwenye mafaili ya MUNGU na ndio unaotoka, na kama ubatizo uliopo mbinguni basi ndio ufuatwe maana ndivyo anavyotaka aliuandaa kwa ajili yako. Ili upone na sasa kama umekataa ubatizo anao utaka MUNGU na ukabatizwa ubatizo asioutaka MUNGU, haijalishi jina lake linatajwa huo sio ubatizo. Ni ubatizo batili haumuhusu yeye hayo ni mapokeo kutoka kwa waanzilishi waliomkufuru ROHO MTAKATIFU na wapo kuzimu. Nilioneshwa na YESU,  tena ni adhabu kubwa sana, wamefungwa minyororo na YESU, ameniambia YESU tayari hawa wameshakwisha kuhukumiwa hawataniona wana subiri moto siku ya mwisho na wamekufuru ROHO MTAKATIFU na wanateseka sana, na walikataa kumtii MUNGU  wakamkufuru ROHO MTAKATIFU. 

Sasa nakushangaa wewe unang’ang’ania dini unasema uatakufa na dini ya wazazi wangu. Dini salama ni YESU tu kupitia wokovu na uwe umeokoka, siyo unajiita mkristo halafu haujaokoka, wewe ni feki mbele za MUNGU, mtegemee yeye tu na utapona,. Ubatizo wa kweli lazima taratibu zote alizozifuata mwasisi wa kanisa zifuatwe Yaani YESU. Ikiwa na maana alichokifanya YESU ni salama na ndio kweli na alifanya ili sisi tufuate njia aliotuonyesha.

Mtoto mdogo abarikiwe kwa kuwekwa wakfu kama YESU, alivyowekwa wakfu na kubarikiwa akiwa Mtoto.

MUNGU aliandaa kumpa ujumbe mtumishi wake Simon, ukisoma katika kitabu Luka 2:29 YESU alivyobarikiwa alikuwa mototo tena ajijui na alivyokuwa mtu mzima anayo fahamu alibatizwa, na huo ndio mpango wa MUNGU wa kweli uliopo mbinguni na hata Yohana alitimiza na YESU akafanya hivyo hivyo. Na kama unataka kuwa mfuasi wa YESU ni lazima ufuate taratibu zote hapo utakuwa kama yeye na utapokelewa na kufurahia nakufurahia na wazee 24 na malaika wake na serikali yake yote ya mbinguni inafurahi.

Huo ubatizo mwingine hawafurahii kabisa na ameniambia waambie wanangu wanielewe, nawapenda. Hayo hayajatoka kwangu maana sasa naukomboa ulimwengu. Maana watumishi wengine vichwa ngumu, wamenisaliti, wamenigeuka ndio maana ulimwengu unaangamia

FAIDA ZA UBATIZO WA KWELI.

Ubatizo wa kweli ni ubatizo wa MUNGU kwa hiyo unamamlaka, unashiriki ubatizo alioutaka MUNGU BABA muumba wa vitu vyote ukiwemo na unashiriki kiapo kamili kama YESU kwa pendo hilo wewe na YESU na wazee 24 wote wanashiriki na zaidi utajazwa ROHO MTAKATIFU kama YESU alivyoshukiwa anakuwa kiongozi wako milele na atakaye kupeleka mahali alipo MUNGU kama YESU alivyopelekwa tena, kwa kushiriki hatua alizozitaka yeye mbinguni utakuwa wazi soma katika kitabu cha Yohana 3:5-7.

HASARA ZA KUBATIZWA KINYUME NA MUNGU
Hasara moja wapo wewe unakuwa unashiriki jambo ambalo halipo mbinguni na hata kitabu cha mwongozo wa kwenda mbinguni yaani biblia.

Jambo lingine unakuwa unashiriki kuvunja Amri za MUNGU soma katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 5:8-9 na Kumbukumbu la Torati 6:14 pia unabeba laana. Unamjaribu MUNGU maana unatumia jina lake na unafanya kinyume na yeye anavyotaka na ukifanya kinyume na yeye tayari unaabudu miungu mingine, kwa hiyo ubatizo ule ambao MUNGU hajauagiza hivyo unaabudu miungu, na wewe ni mwana wa miungu wala si wa MUNGU kwa sababu hujapokea kiapo cha MUNGU kupitia ubatizo wake wa maji mengi, bali umepokea ubatizo ambao haupo kwenye biblia, hivyo ina maana ni ubatizo wa mungu asiyejulikana ambao ni miungu maana haujatoka kwake.

Na usitegemee utaenda kwake sababu una chapa ya miungu, na hao wanaofanya kazi hiyo hawafanyi kazi ya MUNGU kupitia neno lake, bali wanafanya kazi ya kuwapoteza watoto wa MUNGU kupitia maneno ya miungu; kwa mfano ya ubatizo huu wa maji ya kikombe na mengineyo.

Mtoto anapokuwa katika misingi isiyo ya MUNGU wa kweli haijalishi jina la YESU limetajwa au kutumika, mtu huyu ataishi kwa kushikiliwa na shetani na ndio maana mtoto mpaka awe mtu mzima, mpaka unajuta kwa nini umemzaa anavuta bangi, anakuwa mwizi, mtukutu ni mtu wa ajabu hivi vyote sababu ya kwenda kinyume na ubatizo alioutaka YESU, kwa sababu mtoto alitakiwa apelekwe kanisani akiwa mdogo awekewe wakfu, sasa hajapelekwa kuwekwa wakfu.

YESU alibarikiwa akiwa mtoto sasa siku hizi mtoto anabatizwa kwanza halafu akiwa mtu mzima anabarikiwa Je huo ndio mpango wa MUNGU Jibu ni Hapana, mtoto angekuwa amewekwa wakfu kama YESU haya mabaya yote hayampati. Angeanza na baraka na ndio msingi wake MUNGU.

Shetani anakutengenezea kosa ili uangamie, anakushitaki tena. Unaona jinsi alivyo mnafiki na shetani ni mbaya sana mkatae. Anakutengenezea kitu halafu anakushitaki shetani ni mbaya sana mkatae.

Hasara nyingine hauendi mbinguni unakuwa umeshiriki kiapo ambacho siyo kiapo amekitaka yeye MUNGU ili ukombolewe na kama MUNGU hakubali kupokea kiapo ambacho yeye hajalitoa kwake, nikuulize swali Je utakubali kusaini mkataba ambao wewe wenyewe kibinadamu haukuhusu wewe, Jibu hausaini ndivyo ilivyo kama MUNGU. Hasaini wala hakubali.

Hasara nyingine ule wakati na wewe wa kubatizwa ndio unapelekwa kubarikiwa ukiwa mtu mzima, hapo majira yako na baraka zako kwa MUNGU kwako inakuwa imepitwa na wakati. Na MUNGU alikupangia hauendi na wakati ndio maana kuna majira ya kupanda na kuvuna, kuna wakati wakulia, wakati wa kucheka. Kwa hiyo haupati kitu kutoka kwake.

Hasara nyingine wewe unakuwa wa dini na wa sheria tu, na hapa tunajua kabisa dini siyo mpango wa MUNGU na MUNGU anafuata sheria na hapana jambo lingine.

Hasara ya kubatizwa ubatizo ambao si wa MUNGU, unakuwa hutaki wokovu na unakuwa mgumu maana nafsi yako imeshikiliwa na mapokeo ambayo hayajatoka kwa MUNGU, na kama hayajatoka kwa MUNGU, ni mpinga kristo, haiwezekani wewe mkristo halafu unapinga wokovu. Soma katika kitabu cha Warumi 10:9-11 ina maana iko Roho ya mapokeo ya dini na mapokeo ya mwanadamu hayajui yametoka wapi, ni ya shetani na ile roho haimtaki YESU.

YESU aingie ndani yako, huu upofu ambao shetani ametumia njia mojawapo kuliteka kanisa na wewe unayekataa wokovu sasa ufunguke uokoke haiwezekani wewe ndugu msikilizaji unayesikiliza sasa hivi, unajiita mkristo halafu unakataa wokovu umebatizwa huo huo tena zaidi ubatizo wa maji hayo hayo ya kikombe na ubatizo wa maji ya kisima, na ubatizo wa kubatizwa kwa jina la mchungaji. Na unaenda kanisani na umetoa sadaka wewe unampinga na unasema hakuna wokovu hii ina maana kwamba ndani yako iko ile roho ya mpinga kristo, ndio inazungumza na kukataa sasa, ili uokoke lazima hiyo roho ing’olewe, inapoondoka ndio unaokoka na wewe, ukiokoka ndio maana baadaye ulikuwa hauamini, ndio maana unasema haaa hivi nilikuwa wapi, funguka kupitia ubatizo feki, aliyoniambia YESU anakula kiapo na dini na mapokeo yaani yeye ni wa dini tu, siyo wangu na ndio maana mtu huyu hamtaki kabisa YESU ananiambia mtu huyu ananikubali tu mpaka ili roho ya dini na mapokeo itoke maana ndani  yake roho ya kuasi inamshikilia ndani,  na ile kuasi ikiwa ndani yake, haijalishi ni kwa watumishi au waumini.

Atashiriki pombe tena hata atazibariki atafanya uchawi kuoa mke zaidi ya mmoja bila hofu ya MUNGU, na hata ubarikio na ubatizo, na batizo zao watashiriki vitu vya shetani utashangaa mtu siku anabarikiwa na kubatizwa pombe disco sana, sasa nikuulize YESU anashiriki  pombe, YESU anashiriki disco, mapokeo ya nini nikuulize Je YESU anashiriki hayo au ROHO MTAKATIFU anaruhusu disco kwenye sherehe za ubatizo na ubarikio  Jibu Hapana, kwenye hizo sherehe mapepo na roho mchafu ndio huja kushiriki na kufurahi ya kwamba mpango walioupanga kukuangamiza umetimia, wacha sherehe za pombe, disco, haijalishi ni za harusi au nini. ROHO MTAKATIFU huondoka. Roho mchafu huyo hapo..
BWANA YESU ASIFIWE
Tunakuja jambo lingine

Jinsi MUNGU anavyotaka ubatizo ufuatwe, mtoto mdogo akizaliwa apelekwe awekwe wakfu tena iwe madhabahu ya ukweli iliyo hai ambayo YESU anakaa hapo, mtu akiwa na ufahamu aokoke kwa hiari yake mwenyewe, ndio abatizwe kwenye maji mengi tena yanayotembea kijito cha utakaso, siyo kisima tayari imekuwa feki hapo mwili wote uzamishwe kwenye maji, kama YESU alivyobatizwa siyo kichwa au kudondosha kichwani  tayari hujatimiza angalia anaye kubatizwa kweli ana roho wa MUNGU  ndani yake, maana kama roho wa shetani yuko ndani yake hawezi kushiriki ubatizo wa ROHO MTAKATIFU hapo ni ubatizo feki, ubatizwe kwa jina la BABA, MWANA na ROHO MTAKATIFU, usikubali kubatizwa kwa jina la mtu au kitu chochote tofauti na YESU.

Usikubali kubatizwa na Nabii wa uongo, hapo anakuwekea ma roho yake, mashetani aliye ndani yake ili kukunajisi usiende mbinguni usitoe pesa zako kwa malipo ndio ubatizwe YESU hakutoa ili abatizwe na wewe fanya hivyo hivyo usikubali ndugu msikilizaji mahali popote uliko, hii ni kwa ajili ya watu wote ulimwengu mzima rangi zote aliniambia BABA yangu.

Nami natumika kama chombo tu nikueleze wewe, utafikiri ni Hebron lakini ni MUNGU anasema na wewe umeyasikiliza tu, badilika achana na mambo hayo tupa, badilika achana na mambo hayo mrudie MUNGU.

Ujumbe huu ameniambia YESU ni kwa wote ulimwengu huu, na mtu yoyote ambaye amebatizwa kinyume na MUNGU alivyoagiza, waambie hawaja batizwa na mimi YESU, siyo siri kabisa maana ubatizo huu haujatoka kwa BABA yangu ni ubatizo wa mapokeo, haijalishi wanalitumia jina lake wanaofanya hivyo hukumu inawasubiri, injili imebadiliswa na ndio maana watoto wangu hawanioni, wamefungwa na shetani anayefanya kazi ya uongo kinyume nilivyoagiza  anakuwa nabii wa uongo.

Mtu yeyote akiongoea neno langu au kupunguza huyo ni muongo, sina furaha naye, hata BABA yangu na Malaika wa mbinguni wote hawa hawafurahi na ubatizo wa kikombe, maji ya kichwani

Ole wao mwisho wao umefika, narudi kuchukua ulimwengu na kuwakomboa watu wangu mwenyewe na Tanzania sasa ndio Eden, mimi MUNGU nimeichagua, na mataifa yote yatakuja kuponea hapa na kunijua mimi YESU, haya maneno aliyoniambia nimeyanukuu kama alivyoniambia sijaongeza, sijapunguza.
BWANA YESU ASIFIWE
Ooh MUNGU atusaidie sana, nimekuwa nikieleza watu kuhusu ubatizo huu, sasa kuna jambo moja nitakuuliza, watu wengine wanasema kuwa Ubatizo ni Imani yako, ndio imefanya upokee ubatizo ukiwa mtu mzima wewe ulivyopelekwa kubatizwa ukiwa mtoto mdogo, kwanza ulikuwa na imani wewe? Ulikuwa unajua kinachotendeka, Jibu wala hakuna Imani kwa hiyo ni feki.

Ulivyokuwa mtoto mdogo ulikuwa unajua unabatizwa, haujijui sasa utaniambiaje ubatizo ni Imani yako? Hautaki kubatizwa kwa maji mengi.
Ila roho ya dini imekushikilia.

Inakuzidishia kujua haujabatizwa kwa sababu ulikuwa hauna Imani kwanza haujui.

Je hawa wasimamizi wako wa ubatizo mwanamke na mwanaume hao ndio ROHO MTAKATIFU wako? Jibu hapana, kwanza unajilaani maana Imani yako inasimamiwa na mwanadamu au kwa lugha nyingine unamtegemea na kumwabudu mwanadamu.

Neno la MUNGU linasema amelaaniwa amtegemeaye mwanadamu.

Amebarikiwa amtegemeaye MUNGU.

Hapo tayari umelaaniwa wacha mapokeo, kama umesikiliza vizuri ujumbe huu wa siku ya leo alioniambia YESU hakuwa na mdhamini wa ubatizo ni ROHO MTAKATIFU alimshukia YESU, sasa nikuulize swali huyo mdhamini ndiye atakaye kuongoza kwenda mbinguni ?

Wewe huyo mwanadamu saa nyingine ni unakuta ni uchafu hana hata MUNGU nakufungua tu, hapo anavuta sigara, anakunywa pombe, bado anakushika mikono anakuwekea roho mchafu anapita hapo, Jibu hakuna rudi ukabatizwe upya iwe mtumishi wa dini mahali hapo, sehemu yoyote ambayo hujabatizwa.

Ukisoma katika ufunuo ole wake aongezaye au apunguzaye, sasa huu ubatizo umetoka wapi? Umeongezwa, wacha nikuulize swali lingine ndugu msikilizaji hao wasimamizi wa ubatizo , mwanamke na mwanaume wapo kwenye biblia? Ni mapokeo ya mwanadamu badilika fuata YESU acha mapokeo ya wanadamu ni ya shetani.

BWANA YESU ASIFIWE
Ooh MUNGU tusaidie

Jambo lingine aliloniambia ni kuhusu mambo yanayokwenda kutokea Tanzania

Kama nilivyokwisha kuwaeleza toka April 2012 YESU, ndiye kaikamata Tanzania, ameiandaa kama Eden. Mataifa yote yatakuja kuponea Tanzania atainua kila kitu na yeye ameingia kwenye serikali, lakini hatatumia watu, hakuna uovu uliofanyika ambao utaendelea tena.

Haijalishi walikuwa wanatumia uchawi, uchawi haufanyi kazi tena,

Kuna mambo yanayoenda kutokea kwanza nitaanza na uchumi.

Katika migodi ya Tanzania ya madini inaanza kurudishwa Tanzania kwenye ulimwengu wa Roho Tayari na itarudishwa kabisa kwa watanzania,

Shirika la ndege, reli na usafiri wa maji. YESU anahudumia hayo ni maandalizi ya kunyanyua nchi kwenye miji ya hapa maana ameumba yeye

Jambo lingine linaenda kutokea na mtaona mabadiliko makubwa sana, nitaanza na Bunge la Tanzania litakuwa na mabadiliko makubwa na baadhi wanashushwa vyeo, viongozi katika Bunge na wengine watashitakiwa na haya yameshaanza na wakati wowote mtayaona kwa macho, YESU anatengeneza nchi ameamua mwenyewe.

BWANA YESU ASIFIWE
Mabadiliko mengine yanayoenda kutokea, baadhi ya mawaziri watatolewa kwa wakati wake. Wala msiseme ni mwanadamu ni MUNGU mwenyewe, pia na wakuu wa mikoa wanaoenda vibaya hivyo hivyo itakuja kwa wakuu wa wilaya hivyo hivyo kwa madiwani hivyo hivyo.
YESU ameamua mwenyewe anaendelea hatua kwa hatua.

Kwa hiyo mnayoyaona MUNGU ameamua

BWANA YESU ASIFIWE
Uchaguzi wowote katika nchi kuanzia mwenyekiti, diwani, ubunge, uraisi atakaye tumia uchawi ili apate hicho cheo, hatapa ameniambia YESU.

Mliokuwa mnamtegemea shetani kupata madaraka sasa ni mwisho mtayaona YESU anasimamia mwenyewe chaguzi zote na haki mtaiona, akaniambia hawa watu wote sisi mimi nimewaumba?

Nitawaonyesha na kuwabadilisha mioyo wakati wa kupiga kura, yule anayetumia uchawi hata kama wanatoa hongo hawatapigiwa kura na haitaibiwa, mimi nimesimama MUNGU mwenyewe.
BWANA YESU ASIFIWE
Na watumishi wanaotumia nguvu za giza wataporomoka.

YESU mwenyewe ndio anafanya kazi hiyo, na yuko tayari kazini anawashughulikia ni ulimwengu mzima.

Mabara yote anarudi sasa amechoka, anayepigana na mimi anapigana na yeye, hawatakaa waniweze, mimi na songa mbele kama YESU, alivyokuwa akipita hivyo hivyo na  itadhihirika MUNGU ameniambia kwa gharama yoyote ataukomboa ulimwengu, wanao kengeuka kiboko cha kipo njiani na wengine tayari na wengine wanaotaka kukimbia nchi ya Tanzania hawataweza huko waliko, Yona alikimbia huko huko alifuatwa na wengine wako katika nchi hizo hizo za kwao huko huko, YESU anawashughulikia huko huko, wataporomoka, YESU yupo kazini, lazima mliofanya uchawi yawarudie nyie nyie.

BWANA YESU ASIFIWE
Ooh MUNGU tusaidie

Jambo aliloniambia niendelee kuwaambia watoto wangu, hiki nikidonda sugu wazidi kuendelea kufunguka mahali popote wanataja jina langu na kuna michango mimi sipo ni shetani yuko hapo, haijalishi mimi wananitaja, maana siyataki haya. Nilikwishaingia kwenye madhabahu nilipokuwa ulimwenguni enzi zangu niliya bomoa bomoa na kuyakataa, sasa yamerudishwa sipo hapo, mnachanga michango mnaita sadaka hiyo siyo sadaka, huo ni unyang’anyi, makanisa yanayo kopa benki, mimi sipo nimesema kwamba msikope wala msidai riba , mimi YESU nimeshakwisha kukataa. Leo imerudishwa roho ya mpinga kristo hiyo. Kanisa linaloabudu sanamu na mnanitaja mimi sipo, au kuabudu watakatifu mimi sipo, nimewaumba mimi nina wivu, nimesema kisiabuduwe chochote nilichokiumba, sasa hata niliowaumba mnawaabudu mimi sipo. Mahali wanapokuwa na ibada ya wafu nimekwisha sema tengeneza maisha yako hapa wewe unaacha kutengeneza maisha yako hapa unategemea kwamba ukifa utafanyiwa ibada ya wafu, ukisha kata kauli tu, ndio mwisho wako mwana wa MUNGU.
Ooh MUNGU tusaidie, funguka mwana wa MUNGU, kubali kwenda mbinguni usipoteze muda wako hapa, ukisubiri kwamba ukifa utaombewa hii ni usanii tu.
Soma katika kitabu cha Waebrania 7:20 kwa kuwa haikuwa pasipo kiapo Waebrania 9:27.

BWANA YESU ASIFIWE
Anasema kwamba na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja baada ya kifo ni hukumu ooh funguka mwana wa MUNGU, ukisha kufa tu pap, hukumu hiyo yale yote uliyoyapanda ndiyo hayo hayo utavuna hayo, funguka tengeneza maisha yako.

BWANA YESU ASIFIWE
Funguka funguka kabisa, usikubali kabisa “BWANA YESU ASIFIWE”

Jambo lingine hii kwa kanisa lolote linalonyang’anya mali, kusema mimi mnanyang’anya mali zao kwa kutumia jina langu, mimi si mnyang’anyi au mtumishi anayenyang’anya mali kwa kutumia jina lake, huyo sio mtumishi wangu yeye hakutuma watumishi wanyang’anyi, hakutuma watumishi kukusanya pesa , hakutuma kuzini na kondoo, hakutuma kufanya kazi hiyo, inamaana mtumishi wa YESU ndani yake ndiye YESU anayekaa, sasa kama YESU anakaa ndani yake, Je YESU atazini na kondoo? YESU atakunyang’anya mali zako? Je YESU atasema hili ni kaburi, Kaburi la kuzini hapa?

Ooh ninakwambia ameniambia tena ufunuo mwingine hata kaburi alilozikwa halifai kwenda kuabudu pale hilo kaburi, kulisujudia ni yeye peke yake anatakakiwa watu wengine wanatembeza makaburi wanasema YESU hapa, hakuna, hataki acheni hata kuabudu kaburi la YESU hataki liabudiwe ni MUNGU peke yake. MUNGU wa Ibrahimu na Isaka.

Jambo lingine akaniambia mwanangu hivi kuna mtu anaweza kununua nguvu zangu, nikabaki nikiduaa nikamwambia hapana akaniambia hivi leo hii watu wanaambiwa upako wangu unauzwa  ukisikia mtumishi anasema upako unauzwa huo ni upako wa shetani.

Nikuulize wewe kuna mtu anaweza kununua nguvu ya MUNGU. Jibu ni Hapana,
Nikuulize wewe kuna watumishi wanaponya kwa kutumia nguvu za mapepo Je? MUNGU anaponya kwa kutumia mapepo? Funguka ufahamu kaniambia siku hizi mimi mwenyewe nakataa ushoga lakini wameibuka watu ambao wanatumia Jina langu wanasema ndoa za mashoga, sasa nikuulize swali wewe YESU anaruhusu ndoa za ushoga.

Ameniambia YESU huko hayupo na msitegemee akuongoze, nyakati hizi ni mbaya mwana wa MUNGU.

MUNGU akubariki sana.


SALA YA TOBA
BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote nilizozifanya kwa kujua au kutokujua namkataa shetani na kazi zake zote, naomba uniandike jina langu ndani ya kitabu chako nishike mkono uniongoze wewe mwenyewe, nisipotee tena wewe ndiye salama. Amen.

Nakufunika kwa damu ya YESU WA NAZARETI.

Karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE.

Visit www.prophethebron.org na YouTube ya Prophet Hebron.


NABII HEBRON.