Pages

Wednesday, December 31, 2014

SALAMU ZA MWAKA MPYA 2015 KWA MATAIFA YOTE!

BWANA YESU ASIFIWE, YESU WA NAZARETI aliye hai, nawasalimu wote wa mataifa yote nikimaanisha nchi zote sababu nchi zote ni mali ya MUNGU na siyo mali ya shetani. Katika mwaka huu 2015, nilipokuwa naongea na MUNGU yapo aliyonieleza kama mimi mwenyewe Nabii Hebron kwa utukufu wake MUNGU mwenyewe, na yapo ambayo ni ya kuwajulisheni watu wote, wote mjue MUNGU anataka nini na hataki nini. Akaniambia, Hebron mimi sipendi miungu sababu miungu ni shetani, waeleze watu ukweli sababu wengi wananipenda mimi lakini hawajielewi wapo katika upande wa mungu yupi, na haya yote yanasababishwa na watumishi waliomsaliti MUNGU wakawapeleka wanadamu katika ibada za miungu. Sasa nitakuelezea ili uelewe miungu ni nani na MUNGU ni nani. Nitakuelezea kwa kiroho, kila mtumishi anayebatiza ubatizo tofauti na wa maji mengi yanayotembea, tayari yeye anaabudu miungu na hata hilo kanisa silo la MUNGU wa mbinguni bali ni la miungu, haijalishi likatajwa jina la YESU wewe angalia je wanalitenda neno kazi kama lilivyo au ni kinyume? Na utakapoona ni kinyume basi sasa elewa hapo ni kwa miungu na wewe ufunguke ili uwe mwana wa MUNGU na siyo wa miungu.

A.    KAMA UNASHIRIKI YAFUATAYO UJIJUE WEWE UPO UPANDE WA MIUNGU NA SIYO KATIKA UPANDE WA MUNGU WA IBRAHIM, ISAKA NA YAKOBO:

·        Kama haujaokoka na unajiita wewe ni mkristo, bado upo katika miungu.

·        Kubatizwa ubatizo wa kisima, ubatizo wa kikombe, kubatizwa kwa jina la mchungaji.

·        Kumuabudu mtumishi yeyote hata kumuita yeye ni MUNGU.

·        Kubatiza watoto wadogo, kubariki watu wazima.

·        Kanisa lenye huduma sita badala ya tano alizozianzisha YESU au kanisa lenye huduma zaidi ya tano na kuendelea ikiwemo huduma ya Askofu. Hakuianzisha YESUna kama hakuianzisha YESU kaianzisha nani? Jibu, miungu. Na unapoongozwa na mfumo huo na wewe unafanyika kuwa katika mpango wa miungu kama ulikuwa hauelewi sasa uelewe. Amenituma MUNGU niwaeleze ukweli, anayetaka kupona atapona, atakayekaza shingo Jehanamu palipoandaliwa moto wa kuwachomea miungu na wewe usipowacha utaenda huko huko.

·        Kanisa linalofanya biashara, kuwa na benki, kuchangisha pesa makanisani, kukopa pesa benki, hayo yote siyo makanisa ya MUNGU wa kweli bali ni ya miungu, na waumini mnaosali hapo na nyie hufanyika kuwa watoto wa miungu japo haupendi, sasa ufunguke. Ukisoma katika biblia ya Neno la MUNGU aliyeiumba mbingu na dunia yeye anayekataa hayo katika neno lake. Sasa endapo mtu ataivunja sheria ya MUNGU basi ajielewe ameipokea sheria ya miungu na yeye yupo chini ya miungu katika ulimwengu wa roho. Sasa mfunguke mataifa yote, mtoto wa MUNGU ambaye ni YESU WA NAZARETI, karibia anarudi kuja kuwachukua wale ambao wapo katika upande wa MUNGU ambaye ndiye BABA yake yeye hatamruhusu yeyote ambaye yupo katika upande wa miungu, nimekufunulia uelewe jinsi ya kuielewa miungu inavyoliendesha kanisa na kulijenga kanisa lake katika ulimwengu wote na kushika kasi katika nchi zote 98% ya ulimwengu wote, madhabahu zote ni za miungu ya dunia hii.

·        Mahali popote ambapo watu wanaenda kutoa sadaka zao kwa vinyago makanisani au katika kanisa ukaona sanamu ya aina yeyote, hapa uelewe ni madhabahu ya miungu na ndiyo iliyowateka watu hao wasiende mbinguni na bila kutoka hapo uelewe wewe ni adui wa MUNGUwa kweli na unabakia kuwa rafiki wa miungu. Sasa uelewe na ufunguke ufahamu wako (soma katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati 5: 7-9) hiyo ni miungu yenyewe na sasa inayatumia makanisa mengi katika ulimwengu wote na kuwapoteza watoto wa MUNGU kama ilivyo sasa hata wewe fikiria upate picha hizo sanamu ni za nini katika nyumba za ibada? Je kama huyu MUNGU wa kweli yeye anaonya hataki sanamu, je nikuulize swali je anavifurahia viwepo katika madhabahu yake? Jibu, MUNGU aliyeziumba mbingu na dunia yeye siyo MUNGU wa vinyago au sanamu, bali miungu ndiyo inayoshirikiana na vinyago au sanamu katika makanisa au madhabahu

Mahali pa jinsi hiyo uelewe ni kwa miungu. Shetani alitumia ujanja mwingi ili kuwapofusha wanadamu wasijielewe akawateka kama ilivyo wote wanaoshiriki mambo hayo tayari wao ni watoto wa miungu na wametekwa na miungu. Amenituma MUNGU na serikali yake niwafungue macho muelewe ili mpone. Mtoto wake ambaye ndiye YESU WA NAZARETI muda wowote, siku yeyote isiyojulikana hii ni siri yake MUNGU peke yake.

·        Kanisa ambalo kiongozi wake ni mchawi au anatumia nguvu za giza au yeye ni freemason au mwanachama wa illuminati, kanisa lote pamoja na waumini wote wanakuwa chini ya miungu yake huyo kuhani, sababu jinsi alivyo kuhani ndivyo na kondoo wake walivyo.

·        Kanisa linaloongozwa na mchungaji halafu bado yeye ni mwanasiasa au anamtumikia kaisari, huyo ajielewe yeye yupo kwa Kaisari na siyo kwa MUNGU. Hawezi kuwatumikia mabwana wawili, kama ni MUNGU basi ni yeye tu na siyo kujiita mchungaji halafu upo katika siasa wewe haufai mbele za MUNGU. Kila alivyo hivyo yeye siyo mtumishi wa MUNGU bali yeye ni wa miungu. (Kumbukumbu la Torati 6:13-15 soma).

·        Ibada za misalaba, ibada za wafu, kubusu sanamu, kubusu misalaba, hayo yote uelewe ni mambo ya miungu.


NOTE:
Nimeelezea kwa ufupi mpate kuelewa ni jinsi gani miungu ilivyowashikilia watu wengi na hata watumishi baadhi yao hawajui wanaabudu miungu tayari na tayari wameshatekwa na shetani. Katika salamu za mwaka mpya wa 2015 kutoka kwa Nabii Hebron, ikatae miungu ili upone na uchukue maamuzi kutoka katika moyo wako na usishiriki katika makanisa ya miungu, wewe chunguza hayo niliyokueleza na zaidi endelea kusoma katika makala ya Nabii Hebron utaujua ukweli zaidi na utakuwa huru.

Watu wengi wanaona wapo sahihi na hata wameokoka kumbe wapo kwa miungu. Na haya yote ni shetani anaungana na watumishi waliomuasi MUNGU sasa wanatumia jina la YESU kuwapotezea watu na kumbe siri wanaijua.

Sema BWANA YESU WA NAZARETI naomba unisamehe dhambi zangu zote unitoe kwa miungu uniandike katika kitabu chako cha uzima wa milele. Miungu siwataki katika maisha yangu pamoja na madhabahu zenu kimwili na kiroho. Amen.

Karibuni katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE mkutane na MUNGU aliyeiumba mbingu na nchi pamoja na wewe na awe MUNGU wako sasa.


NABII HEBRON.