DALILI
ZA KULIJUA KANISA NA MTUMISHI ANAYEONGOZWA NA ROHO MCHAFU 100%.
Kama nilivyokuisha kusema katika makala ya dalili ya kulijua
kanisa linaloongozwa na ROHO MTAKATIFU, hivyo hivyo na shetani na yeye alituma
msaidizi wake ili kuja kuwasaidia wale watakao kataa kufuata kweli na
kuwasaidia kuwapeleka jehanamu. Kazi ya roho mchafu ni kazi ya mpinga kristo
ambayo kazi yake ni kulibadili neno la MUNGU kama vile ilivyo sasa katika
mataifa mbali mbali, watu wanajiita ni wakristo lakini kumbe ndiyo maadui
wakubwa wa MUNGU sababu ya kuongozwa na roho mchafu kwa njia ya kuwapiga watu
upofu wanatumia biblia lakini wanachanganya ya kweli na ya uongo. Na tukijua
kuwa nuru na giza hawachangamani au YESU na shetani hawana ushirika ila biblia
inatumiwa makanisani halafu na mengine yanaongezwa, inapokuwa hivyo tu uelewe
hapo yupo pepo au roho mchafu ndiye anayesimamia kuwaongoza na kuwasimamia hilo
kundi ili alipoteze kwa kwenda jehanamu. Nitaelezea mambo machache ya kuelewa
kanisa au mtumishi anayeongozwa na roho mchafu na mtapona sababu watu
wanafikiri wanaongozwa na ROHO MTAKATIFU kumbe ni roho mchafu anajaa sehemu
nyingi katika ulimwengu wote.
·
Inawezekana mtumishi aliitwa na MUNGU kabisa ila
alipomsaliti YESU tu basi anakuwa anaongozwa na roho mchafu.
·
Watumishi wake huteuliwa na wanadamu na pia
hawajaitwa na MUNGU wala hajawahi hata kusikia akiitwa na MUNGU, hawa
wanajiita, wanatafuta pesa au mishahara tu.
·
Kanisa hilo ni lazima libatizwe ubatizo ambae
siyo YESU alibatizwa nao na siyo ubatizo wa Yohana wa maji mengi yanayotembea
na yamejaa tele wala siyo ya kisima, hapa tayari roho mchafu amepindua neno la
MUNGU.
·
Utakuta mtumishi anabatiza kwa jina lake iwe ni
ubatizo wa maji mengi au ya kikombe.
·
Wanabatiza watoto wadogo na kubariki watu wazima
(hii ni tofauti na biblia).
·
Watumishi wake wanavaa kofia, wanaingia na fimbo
na mikuki kanisani wakati biblia inakataa.
·
Wanaabudu wachungaji kama ndiye mungu wao na
wengine huwaita wao ni mungu wa majeshi, mungu mweusi, mungu mweupe, na wenigne
hujiita wao ni YESU.
·
Huta huduma za kiroho kwa malipo mfano wanadai
sadaka ya ukombozi au vitu vyako ndio wakusaidie kama ilivyo kwa mganga wa
kienyeji anavyoongozwa na mapepo anateka vitu vyako.
·
Wanaabudu sanamu, misalaba, kufungisha ndoa za
mashoga, bariki pombe, wanaandika sadaka majina, na email na namba zao za simu
na kiasi.
·
Wanatoa vyeti vya hongera kwa wale wanaotoa pesa
nyingi na kuwasoma madhabahuni wapigiwe makofi.
·
Makanisa yenye watu wanaoitwa partners
(special).
·
Yanakopa pesa na kulipa riba na mengine
yanachaji watu riba.
·
Wanafanya miujiza ya kipepo.
·
Makanisa yao yana nembo za freemason na
illuminati.
·
Wengine viongozi wao ni wanachama wa illuminati
na freemason.
·
Makanisa yana huduma sita badala ya zile tano
alizozianzisha YESU ikaongezewa ya sita ya uaskofu na zipo nyinginezo kwa
majina yake zinafika kumi na zaidi.
·
Walevi, wazinzi, wachawi, wanyang’anyi na
kutenda ufisadi.
·
Watumishi wake ili umuone lazima utoe pesa na
wengine ili umguse ni lazima utoe kiwango fulani cha pesa ndio akuombee au
unayetoa kiasi kikubwa cha pesa utasaini katika suti yake katika mabega yake na
wale wa viwango vya chini wanasaini katika suruali eti ndiyo watakayobarikiwa.
Hawa ni mapepo ndiyo yapo ndani yao yanaiba pesa za watu na roho inayofanya
kazi hapo haina tofauti na roho za wachawi au waganga wa kienyeji. Kiongozi ni
roho mchafu.
·
Kufanya ibada za wafu.
·
Wakati wa kuapishwa kuifanya hiyo kazi wengine
wana lala chini ndiyo kiapo chao.
·
Ni mambo ya dini na sheria kama enzi za
Mafarisayo ndiyo zinaendelezwa.
·
Wanabatizia ndani ya kanisa lipo kisima.
·
Fungisha ndoa za kishoga na kufungisha kwa agano
la shida.
·
Watumishi baadhi wapo katika mtandao wa internet
ni illuminati na freemason.
·
Hakuna kuokoka na wengine wanasema ukiokoka
umepotea.
NOTE:
Hii
yote nimekufunulia uelewe jinsi kanisa la sasa katika dunia yote kiwango
kikubwa sana linaongozwa na roho mchafu kama ndiye msaidizi wa kuyaendeleza
hayo ambayo hayapo katika biblia na kama hayapo basi jiulize yametokea wapi?
Wakati biblia imeeleza neno la MUNGU lisiongezwe au kupunguzwa chochote, MUNGU
amekihakikisha na akaupiga muhuri. Sasa niwaulize je kama MUNGU amepiga muhuri
biblia ndiyo katiba yake ifuatwe na ukienda kinyume ujue umeivunja katiba ya
MUNGU na hata katika nchi yeyote unapoivunja katiba unashtakiwa na kuhukumiwa.
Hivyo ndivyo ilivyo na wakristo wengi na makanisa tayari yamejiingiza katika
hukumu kwa kuongozwa na roho mchafu na adhabu yake imeandikwa katika kitabu cha
Ufunuo 22: 18-19, je na wewe upo upande upi? Sasa utubu sema
BWANA
YESU naomba unisamehe dhambi zangu sikujua kama naongozwa ma roho mchafu na
nikaishi chini ya ufalme wa roho mchafu naomba unisamehe. Uniandike jina langu
katika kitabu chako cha uzima wa milele. Namkataa shetani na roho mchafu kwa
jina la YESU WA NAZARETI nakuunguza uteketee, achilia nafsi yangu sasa hivi. BWANA
YESU nishike mkono na ROHO MTAKATIFU aniongoze na siyo tena roho mchafu.
Niongoze YESU katika kanisa linaloongozwa na roho wako mtakatifu wa kweli.
Amen.
NABII
HEBRON.