JE UNAJUA
TAA YA CHEMLI NI NYUMBA YA SHETANI (JOKA KUU).
BWANA YESU ASIFIWE, watu wote wa mataifa yote karibu sana
katika makala ya Mtume na Nabii Hebron Wilson Kisamo. Ufundishwe na upone na
pia karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, Arusha,
Tanzania. Ingia katika website www.prophethebron.org
utakutana na habari za YESU alizonieleza kwa kinywa chake pia na katika
YouTube.
Mwaka 2010 wakati bado ninafanya kazi ya professional driver
guide, mara nyingi sana YESU alisema na mimi mara nyingi sana, alinifundisha na
kunipa maagizo nimuaandalie kanisa lake la mwisho, akanichukua, akanipeleka
kuzimu, nikaona mahali anapoishi Joka Kuu, yeye ambaye ndiye baba yake shetani.
Nikaiona nyumba yake ilivyo na sasa ni miaka mine tokea YESU anijulishe hayo.
Nyumba ya Joka Kuu ipo kama vile ilivyo ile chupa ya chemli ya kioo,
nilishangaa, akaniambia angalia vizuri sana ila sikujua mimi maana yake.
Ilipita miezi mitatu, karibu itimie miezi mine hivi akanifundisha maana yake
niliogopa sana, na mimi akanionya nisitumie kabisa taa ya chemli sababu
unapoitumia ina maana kuwa katika nyumba yako umeijenga nyumba ya Joka Kuu na
hivyo yeye hupata mlango kupitia hiyo taa. Akaniambia aliwakamata wanadamu
fahamu zao na wao hawajui lengo ni nini ila sasa Hebron wewe ndiye
nimekufunulia mtumishi wangu
Sasa mimi naishi ndani yako na hayo yamefichika, niliowaita
ili niwafunulie mambo yaliyofichika nao wamejiunga na Joka Kuu, ila kupitia
wewe injili yangu itaenda mbele tu na watu watapona. Wale watakaokusikia
watapona na wale watakao kaza shingo hawatapona. Akaniambia, unapoiwasha katika
nyumba yako ule mwanga unakuwa ni mwanga wa joka kuu unamiliki maisha yako na
balaa na mikosi na vifungo vinakumulika kila mahali na hata maisha yako.
Akaniambia tumia mshumaa au torchi au taa ya umeme. Hata kama itakuwa ni taa ya
bulb halafu ikawekewa chemli bado itakuwa tuu umeiweka nyumba ya joka kuu
itawale hapo na maisha ya watu na kila unapotumia chemli unazidi kujengwa
katika nyumba ya joka kuu na katika ulimwengu wa roho na wewe unakuwa unaishi
katika nyumba ile ambayo nimekuonyesha ya joka kuu. Yapo madhara mengi ila
nitayaelezea katika makala nyingine.
Ninakufunulia sasa uelewe na upone hayo ni maamuzi yako wewe
kuacha sababu nimekujulisha asili yake na watu hawajui na ndio sababu watu ni
ngumu kukaa katika utakatifu sababu shetani alibuni ni jinsi gani atamteka
mwanadamu. Ni bora koroboi, ni salama. Wengi mtapona sasa. Mshukuru YESU WA
NAZARETI anayenifundisha na MUNGU wa mbinguni na ROHO MTAKATIFU ili mtoke
kwenye majengo ya shetani. Miji yenu
isiwe ni nyumba ya joka kuu ili MUNGU afanye makao katika nyumba zenu na awe ni
BABA yenu. Utakapoacha kuitumia tu na kuitoa katika nyumba yako kitendo hicho
tayari umeiondoa nyumba ya joka kuu na mikosi yake na kila kitu. YESU
atakaribia katika nyumba yako na atakuwa ni mlinzi wako.
Zaidi soma makala ya Nabii Hebron utayajua mengi na utakuwa
huru, nawakaribisheni mataifa yote katika KANISA LA YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA
MATAIFA YOTE, Arusha, Tanzania. Amen.
NABII HEBRON.