Pages

Saturday, December 23, 2017




MERRY CHRISTMAS 2017 AND HAPPY NEW YEAR 2018.

Kanisa na watu wote nawatakia heri ya krismasi na mwaka mpya 2018. Muwe na krismasi njema na baraka zake ziwe juu yenu katika jina la YESU wa Nazareti. Bila kusahau katika sikukuu hii ya krismasi tunakumbuka siku ya kuzaliwa kwake mwokozi wa ulimwengu huu na cha kujiuliza kwa anayesherekea je unausherekea kuzaliwa kwake Bwana YESU?

Basi ingekuwa vizuri watu waokoke wamkiri yeye kama Bwana na mwokozi wao, siyo kusherekea na kufurahia hiyo siku yake wakati haumkiri kuwa ni Bwana na mwokozi wa maisha yako, maana pasipo yeye, kama MUNGU asingemtuma kuja hapa ulimwenguni sijui dunia ingekuwaje? Hivyo nawasihi mataifa yote muokoke na kumpokea yeye ukimaanisha na unapoisherekea hiyo siku yake zipo baraka ambazo atakupatia wewe uliyeokoka na kwa yule ambaye hajaokoka hawezi kuzipata hizo baraka zake sababu yeye hamtaki halafu anataka baraka zake; ni sawa na mtu hakupendi halafu anataka umsaidie ni vigumu.

Sasa mfunguke fahamu na mzidi kumpenda huyu mwokozi mkimpokea kwanza na yeye atawafurahia sana, siyo tena kubakia kuitwa mkristo halafu hamtaki kuokoka, unajipotezea muda wako utakuwa kama msindikizaji ila kwa safari hii okoka.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele.

Ubarikiwe na ufunguliwe.
Merry Christmas and Happy new year 2018.


NABII HEBRON.