Pages

Thursday, February 26, 2015




(HUYU NDIYE ALIYEMZAA NABII HEBRON KIROHO- MOSES KULOLA)














UKRISTO WENYE ASILI YA KUZIMU UPO HIVI…

BWANA YESU ASIFIWE, YESU WA NAZARETI ambaye ndiye kristo wa MUNGU au mwana wa pekee wa MUNGU aliyetumwa kuja kulikomboa ulimwengu. Katika somo hili nitafundisha uelewe na utofautishe ukristo wenye asili ya shetani au uliotoka kuzimu ukoje na hata sasa upo hapa ulimwenguni kwa kiasi kikubwa sana na ukristo huo umeshikiliwa na kupokelewa kwa kiwango kikubwa na pasipo watu kuelewa kuwa ukristo huo walio nao siyo wa MUNGU bali ni ukristo wa mpinga kristo.

Ukristo huo unaitwa mpinga kristo sababu upo kinyume na YESU, ROHO MTAKATIFU pamoja na MUNGU aliyeumba kila kitu. Ukisoma 1 Yohana 4:1-6. Nabii Yohana alisema wapenzi msiziamini kila roho bali zijaribuni kama zimetoka kwa MUNGU. Hapa ndipo watu wametekewa na mpinga kristo hata na kujiunga na umoja wa mpinga kristo japo najua idadi kubwa zaidi inampenda YESU ila alilolituma adui hapa wakaleta roho yao ya kristo wa uongo, ikaja duniani na ikafanikiwa kuanzisha makanisa wakitumia jina la YESU ili kuwateka wengi hata wale wateule wa MUNGU wakajiunga nao vizazi na vizazi. Pia kumbuka YESU alishasema wengi watakuja kwa kutumia jina langu na watawateka wengi, hata sasa imetimia, ila YESU alishatupa ishara zote, yeye hapaswi kulaumiwa sababu alishayaweka yote wazi wazi.

Cha kujiangalia zaidi ni kuzichunguza hizo roho, je wanachokifanya kimetoka mbinguni au zimeruhusiwa katika neno na ukiona ni kinyume uelewe ukristo huo siyo ukristo wa mbinguni ni ukristo ambao asili yake ni kuzimu na unaposhiriki basi na wewe tayari umeshakuwa mfuasi wa kristo wa kuzimu na hata katika ibada zote uelewe unamuabudu kristo wa kuzimu kabisa, na hata kama ni kanisa linajiita ni la kiroho na unaona umeokoka lakini lipo kinyume na biblia tu uelewe unazidi kujiimarisha katika ufalme wa mpinga kristo wala wewe siyo wa YESU wa mbinguni.

Nitaelezea machache ili upate picha uelewe na ukatae ukristo wa kuzimu:
Ukristo unaobatiza watu kwa ubatizo wa maji ya kikombe, kubatiza kwa maji ya kisima, kubatiza kwa jina la mchungaji, kubatiza watoto wadogo. Tafuta katika biblia ya MUNGU, haya hayajaruhusiwa na kama hayajaruhusiwa sasa uelewe ukweli huo ni ukristo wa kuzimu na siyo wa mbinguni.

Wakristo wanaoabudu sanamu.

Kubariki watu wazima, badala ya watoto wadogo.

Ukristo unaoongozwa na huduma 6 na zaidi badala ya zile tano alizozianzisha YESU.

Ukristo unaoruhusu pombe, ushoga, unazuia watu kuokoka, kutolea sanamu sadaka, kufanya ibada za wafu, kuandika sadaka majina, kumuabudu mcungaji.

Ukristo wenye viongozi freemason, illuminati, mchawi na mengineyo, ikiwemo kuweka misalaba katika nyumba za ibada.

NOTE:
Nimeeleza, naamini utakuwa sasa umepata picha na wewe utafunguka na uwatumie na wenzako ili wawe nao wakristo wa mbinguni kama wapo katika ukristo wa kuzimu watoke wasije wakaangamia. YESU aliye mwana wa MUNGU yeye yupo mbinguni, na ili uwe mkristo wa mbinguni ni lazima uifuate biblia ilivyo na siyo uchanganye ukweli na uongo, inapokuwa tofauti tu uelewe umeshakuwa mkristo wa kuzimu, na kama upo hivyo basi uelewe ukifa utaenda huko kuzimu ambako na wewe umeyashika mafundisho yao. Ila ipo neema ya YESU, amenituma mimi Hebron niwafundishe muujue ukweli na utakapo upokea utakuweka huru kama unavyoelewa sasa kuwa ulishapotezwa upo katika njia ya yesu wa kuzimu. Yesu huyu wa kuzimu njia yake ni uongo na ili kuujua uongo chunguza mafundisho yake hapo utapata jibu, tena bila ubishi.

YESU aliponieleza mimi mwenyewe niliogopa sana sababu hata mimi nilibatizwa ubatizo ambao haujatoka mbinguni yaani ubatizo wa maji ya kikombe nikafanywa niwe mkristo wa kuzimu, lakini YESU WA NAZARETI aliniokoa na kunitoa katika kambi ya ukristo wa kuzimu ili siku moja niwepo mbinguni na yeye alipo. Nawasihi muokoke sasa enyi watu wa mataifa yote, na kama upo katika ukristo wenye asili ya kuzimu nakusihi utoke huko sababu wakristo wa jinsi hiyo wanaandaliwa moto wa kuwachoma milele sababu wamekuwa wapinga kristo. Ila wengi wametekwa hawajijui na wengine wanajijua kabisa wanafanya kazi ya shetani kabisa ya kueneza umissionary wa yesu wa kuzimu ili shetani awateke watu kwa kutumia jina la yesu wa uongo.

Sema BWANA YESU WA NAZARETI uliye mbinguni naomba unisamehe dhambi zangu. Najitoa kwa yesu wa kuzimu na sasa mimi uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele. Sikutaki tena wewe kristo wa kuzimu kuanzia sasa. Amen.

Mpaka hapo umeokoka na wewe ni mkristo wa asili ya mbinguni. Sasa usirudi katika nyumba za ibada za jinsi hiyo tena, wala usishiriki tena, ukiingiza hata mguu wako tu tayari unatekwa tena na shetani. Zaidi fuatilia masomo katika website ya www.prophethebron.org

NABII HEBRON.