Pages

Thursday, February 19, 2015

UBATIZO WA MAJI YA KISIMA NI UBATIZO WA KABURI.

Ubatizo aliobatizwa YESU ulitoka kwa MUNGU wala haukutoka kwa mwanadamu. Ukisoma katika kitabu cha injili ya Yohana 3:1-36, inaelezea vizuri kabisa jinsi YESU alivyobatizwa, na inaelezea YESU hakubatizwa katika kisima bali ni katika mto ambao maji yalikuwa yanatembea yakiwa yamejaa mto tele, ikiwa inayomaana hii unapobatizwa katika mto ni lazima maji yawe yamejaa kiasi kwamba unaweza ukazamishwa mwili wako. Na pia kama YESU duniani alienda mpaka mahali penye mto? Jibu, alijua ubatizo unayotakiwa ambao ulitoka kwa MUNGU ili afanye agano na mwanadamu awe mtoto wake, sasa nawauliza swali, je mnaamini ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni? Jibu, ndio. Je ubatizo wenyewe ukoje? Ni wa maji mengi katika kijito cha utakaso yaani maji yanayotembea, siyo yaliyochotwa au kuhifadhiwa, yakajazwa kwa mikono ya wanadamu badala ya yeye MUNGU kuyaleta akisjirikiana na umbaji wake na siyo kwa kujenga kisima.

YESU alikwisha onyesha njia, sasa yeye ndiye njia salama, sasa hamuoni tayari hiyo siyo njia salama? Ubatizo umebadilishwa. Ila kama alivyonituma YESU mimi Nabii Hebron ni lazima niufikishe ujumbe wake na niufichue ushetani ulioingilia katika tendo la ubatizo na kuwafanya mabilioni ya watu waweke agano na shetani badala ya MUNGU na kufanyika kuwa ni wakristo wa kuzimu hawaendi mbinguni. Swali lingine, imeandikwa MUNGU analihakikisha neno lake na alisema lisibadilishwe na atakaye liongeza au kulipunguza hataenda mbinguni (soma Ufunuo wa Yohana 22: 18-19). Hapo jambo la kwanza unaona wazi wazi huu ni uongo wa shetani sababu siyo kijito yaani maji yanayotembea bali yamesimama haijalishi yamejaa tele. Swali, je yanatembea? Jibu, hapana. Je hicho kisima ni kazi ya MUNGU kulitengeneza au ni kazi ya mwanadamu, jibu ni wanadamu wamejenga. MUNGU angetaka watu wabatizwe katika kisima angemtuma Yohana, lakini hakutaka.

Sasa niwaulize mnataka aliyotumwa Yohana au ubatizo wa kazi za wanadamu? Taka wa Yohana ili upone. Ila ipo siri kubwa sana ambayo shetani ndiye na yeye alimtuma mjumbe wake ambaye anaitwa Yohana wa kuzimu na yeye ndiye aliyeuleta huo ubatizo wa maji ya kisima akawapiga upofu watu ili waone wamebatizwa katika maji mengi kama ilivyo katika biblia lakini mpaka sasa umeelewa. Hivyo nakushauri ubatizwe upya wewe umepokea ubatizo wa agano la shetani. Ubatizo wa maji ya kisima unazo siri za shetani na mimi Nabii Hebron nitakueleza sababu ninataka kusudi la BABA yangu aliye mbinguni tu ndio litimie na hili la shetani nilibomoe na watu waende mbinguni.

Ubatizo wa maji ya kisima unapokuwa umezamishwa pale unaingizwa katika kaburi katika ulimwengu wa roho, umezikwa na vitu vyako na kufungiwa katika hilo kanisa lenye agano la ubatizo ambao haujatoka mbinguni.

Jambo lingine, katika makanisa ya kiroho 99.9% ya watumishi wanaotumia ubatizo wa kisima huwa tayari ni wachawi na huwa ni watenda kazi wa shetani kabisa ila wanajificha kwa kujiita watumishi na hata ndio sababu nyingine hawa katika makanisa ya kiroho wanawabatiza waumini kwa majina ya wachungaji. Lile ni agano la shetani na unapobatizwa hivyo unakuwa wewe ni mali ya shetani na hata kama mpaka sasa na wewe umebatizwa hivyo uelewe mbinguni hauendi sababu unalo au uliingia agano la ubatizo wa kisima au la kuua roho yako na kufungwa utumikishwe na mchungaji huyo badala ya YESU siku zote za maisha yako na siku ya mwisho YESU ataliangalia agano la ubatizo ataona ni tofauti basi utatupwa katika ziwa la moto.

Asilimia 1% ndiyo makanisa yameiga huo ubatizo pasipkujua ila nawaeleza hata wewe uliyeiga haukuiga katika biblia bali umeiga kutoka katika kazi za wanadamu hivyo shetani bado yupo na wewe sababu ananyanyua mashtaka kwa MUNGU si amebadilisha ubatizo, na MUNGU ananyamaza sababu ni kweli. Tubu mkabatizwe upya, bado hauna agano na YESU wa mbinguni bali lipo agano la shetani kwako.

Maji hayana uhai ni maji mauti.

Ubatizo huo ndio agano la freemason, illuminati, na mpinga kristo na kwa wale watumishi wanaobatiza hivyo nao hupewa nguvu na shetani ili kuweza kuliendesha kanisa hilo na kuwafanya watoto wa MUNGU misukule au vitega uchumi vyao. Ili amkamate muumini awe teka wake ni lazima akuzike kwa njia ya ubatizo wa kisima. Na ndiyo sababu wengi wanateseka na mambo kuwa shida, kumbuka ulipobatizwa, ulizikwa na haiwezekani ufufuke ni mpaka uje ubatizwe tu ndipo ufufuke na uingie agano na YESU, na pia ubatizo wa kisima unakufukuzia mbali na YESU na kukukaribisha katika ufalme wa shetani.

NOTE:
Batizo zote tofauti na ubatizo wa Yohana ni batizo za shetani alizozituma huku duniani na zimepokelewa na ule wa mbinguni umekataliwa ili wanadamu wasiwe watoto wa MUNGU. Amenituma YESU kwa sauti ya uchungu, Ole wao wanaowapoteza watoto wangu. Nenda uwaeleze, watapona wale watakao tii, shetani anajua ile siku ya mwisho wapo wengine hawatendi dhambi ila atawahstaki wanalo agano la ubatizo wa shetani. Sasa nawaeleza wakati ndio huu sasa, uje utolewe hilo agano, ili ile siku ya hukumu usiwekewe shtaka na shetani. Zaidi soma masomo ya ubatizo katika blog ya Nabii Hebron, na pia sikiliza mafundisho katika YouTube ya Prophet Hebron, na watumie na wengine ili wapone. YESU anarudi, usikutwe na agano la shetani na usishiriki hata kuabudu katika sehemu wanayobatiza ubatizo wa kisima, hapo ni makao ya shetani na huo ni mlango wa shetsni. Na pia kisima hicho ni lango la kuzimu, wewe ulipelekwa huko.

Sasa sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, uniandike jina langu katika kitabu chako cha uzima wa milele. Uniongoze nikaondolewe hili agano la lango la kuzimu, katika nafsi yangu ili niingie agano na wewe YESU sababu mpaka sasa halijatoka. Amen.

Ufanye haraka ubatizwe upya na ukatengwe nao. Karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE ubatizwe uwe huru.


NABII HEBRON.