Pages

Saturday, February 7, 2015

SANTA CLAUS AU SAINT NICHOLAS HUYU NDIE MWANADAMU ALIYEMUIBIA YESU UTUKUFU WA SIKU YA KRISMASI (BIRTHDAY).

BWANA YESU WA NAZARETI ASIFIWE. Nawasalimu watu wote mnaompenda YESU au kwa jina lingine anaitwa Nabii Issa. Nabii ambaye ndiye aliyeteuliwa na MUNGU kama njia ya kutupeleka mbinguni bila yeye haufiki sababu hakuna aijuaye njia hii ya kwenda mbinguni hata mitume waliopo na waliopita. Ndiye Nabii ambaye mpaka sasa katika ulimwengu huu jina lake ndilo lenye nguvu kuliko majina yote na ndiye Nabii katika ile siku ya mwisho yeye ndiye aliyeteuliwa kuja kuwanyakua wale watakatifu na ndiye atakayehukumu ulimwengu huu, na zaidi hata biblia imemtaja yeye ndiye mwana wa pekee wa MUNGU aliye hai, hivyo ni wa kuheshimiwa kuliko chochote katika ulimwengu huu na kupendwa.

Ila cha ajabu shetani katika miaka ya nyuma akawaingia wanadamu kupitia Santa Claus au Saint Nicholas wakawaita wao ndiyo Father Christmas badala ya YESU WA NAZARETI aliye BABA yetu iwe ni siku yake maalum na kumtukuza MUNGU kwa kutuletea mkombozi ikabadilishwa na wapinga kristo na waliompinga MUNGU na matokeo yake sasa kila Krismasi watu wamewachanganya Santa Claus na Saint Nicholas kama ndiyo siku yao badala ya kuwa ni siku maalum ya YESU. Watu walitekwa fahamu zao na kanisa ambalo halikumsikiliza MUNGU au kulitetea jina la YESU  na lenyewe likajiunga katika upande wa Santa Claus na Nicholas. Ila sasa aliyonituma mimi Hebron katika ulimwengu wote niwaeleze ukweli, utakayesikiliza utapona, utakaye kataa kusikiliza utaangamia. Wakristo wamepotea kiasi kwamba ile siku ya mkombozi wao ambaye ndiye YESU hakuna mpaka sasa aliye thubutu kutaka siku ya kuzaliwa YESU kuwa ni siku yake wala haipaswi kushirikishwa na chochote. Ila YESU amedharauliwa sana hata MUNGU aliye BABA yetu na aliyeumba vitu vyote amedharauliwa na huu ndio ukweli lazima watu wafunguke ili wasijewakapelekwa jehanamu.

Siku ya Krismasi ilipoingiliwa na huyu mwanadamu anayeitwa Santa Claus au Nicholas shetani ndiye aliyeandaa jambo hili sababu hakufurahia YESU kuzaliwa na ili kuivuruga ile siku akawateua Santa Claus na Saint Nicholas, na watu wakaamini mpaka sasa na imekamata dunia yote. Sasa kinyume chake unapomtaja Santa Claus au Nicholas unakuwa unaabudu aina ya mungu anayeitwa Claus na unapokuwa unamtaja Santa Claus inakuwa yeye ndiye anayekutawala katika ulimwengu wa roho wala MUNGU hakupati sababu unakuwa unalo shtaka ambalo shetani analinyanyua kwa MUNGU juu yako kuwa huku duniani una vitu vyake mfano father Christmas, kadi zake, picha zake na hata unapiga picha na yeye. Sasa muelewe watoto wa MUNGU, hii ndiyo njia nyingine pia aliyoitumia shetani na akafanikiwa kwa liasi kikubwa kuiteka dunia, hakuna mahali ambapo Santa Claus hatajwi wakati wa Krismasi.

Sasas jiulize je ilikuwaje na ina maana gani yeye atajwa kama ndiye mhusika wa siku hiyo? Natumaini umeelewa na utapona. Yapo mengi aliyoyafanya Santa Claus katika ulimwengu wa roho japo alishakufa sasa hivi ni mzimu na hajaenda mbinguni nimemuona kuzimu na nilimfanyia kile alichonieleza YESU sababu huyu ni adui wa YESU. Tazama Petro hakukubali YESU achezewe alikata sikio la yule Myahudi, na wewe usikubali kabisa jina la YESU lichezewe kwa kutumika kwa uongo sema kweli tu siyo upige mtu. Vita vyetu ni vya kiroho siyo vya kimwili. Sasa na wewe unaposhiriki katika Krismasi na Santa Claus na wewe unakuwa umeungana kuiba utukufu wa MUNGU na kuwapeleka watu wampatie shetani utukufu eiza kwa kujua au kutokujua. Sasa tazama kanisa lilivyotekwa na shetani lenyewe ndiyo kiongozi wa kumtaja huyu Claus na Nicholas ambaye hana tofauti hata na wewe.

Sasa uache ili upone na wewe unayetaka kwenda mbinguni inakubidi umkatae kuanzia sasa huyu Santa Claus ili ile siku ya mwisho usiwe na shtaka ulilowekewa na shetani na wewe haujui ukakutwa unayo hatia. Na kama mpaka sasa  unavyo vitu vya Clause au Nicholas ujijue unalo shitaka ambalo shetani analificha pasipo wewe kujua ili ile siku ya mwisho atasema na wewe au yule alishiriki kuifanya siku ya kuzaliwa YESU kuwa ni siku ya Santa Claus pia na ukaiunganisha na yeye. Hilo ni kosa na ni dhambi na ujue unakuwa unamtukana MUNGU unapoifanya siku ya mtoto wake kuzaliwa na kuiita Santa Claus, hata kutengeneza mdoli anaitwa father Christmas. Hii ni sawa na huyu father Christmas (mdoli) eti ndiye MUNGU, je MUNGU ni mdoli? Ili mpone achaneni na mambo ya Santa Claus na father Christmas kabisa. Zaidi ingia katika YouTube ya Prophet Hebron nimeelezea zaidi kuhusu father Christmas na pia katika blog hii ingia kupitia website www.prophethebron.org.

NOTE:
Je, Huyu Santa Claus ni mwana wa pekee wa MUNGU? Je, Yeye ni Emanueli? Je, yeye alizaliwa na Maria? Je, yeye alizaliwa kwa uwezo wa ROHO MTAKATIFU? Je, yeye ndiye Kristo? Je, yeye ndiye Masiya? Je, yeye alikufa na kufufuka. Mpaka hapo umepata picha ya kuwa huyu ametumiwa na shetani kuiba utukufu wa siku ya BWANA YESU kuzaliwa na kuwapoteza watu wote wanaomuamini yeye.

Sema BWANA YESU WA NAZARETI, naomba unisamehe niliabudu miungu, nikashiriki kuchafua siku yako ya kuzaliwa, naomba uniponye sasa. Sitaki tena mambo ya  Santa Claus nakutaka wewe tu hata vitu vyake sivittaki tena milele. Amen.


NABII HEBRON.