KILA
ANAYESHIRIKI KUWA BABA WA UBATIZO AU MAMA WA UBATIZO AJIELEWE ANAMKUFURU ROHO
MTAKATIFU AU ANAMTUKANA MUNGU.
Nawasalimu watu wote wa mataifa yote kwa jina la YESU NI
BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE yeye ambaye alikuja ili tupone kupitia yeye.
Ukisoma
katika kitabu cha injili ya Mathayo 3: 16-17 “16 Naye YESU
alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu
zikamfunukia, akamwona ROHO WA MUNGU akishuka kama hua, akija juu yake. 17
na tazama, sauti kutoka mbinguni ikasema, huyu ni mwanangu, mpendwa wangu,
ninayependezwa naye.”
YESU alipobatizwa kwanza alienda peke yake katika maji
hakusindikizwa na mtu ili abatizwe, na alipotoka katika maji baada ya kubatizwa
alilakiwa na ROHO MTAKATIFU ambaye ndiye aliyemsimamia YESU katika ubatizo. Na ndivyo
inavyotakiwa unapobatizwa hakuna kusimamiwa na mtu yeyote awe ni mwanamume au
mwanamke, ni ROHO MTAKATIFU peke yake na hauwezi ukamuona hata ROHO MTAKATIFU
kwa sura yake, japo wengine wamewadanganya watu ROHO MTAKATIFU ana sura kama ya
njiwa, huo ni uongo. MUNGU alitumia njia ya kuwajulisha wale kwa kutumia kiumbe
chake aina ya njiwa kutoka mbinguni, sababu nataka mjue pia mbinguni wapo
wanyama na mimi niliwaona. Ila nilishangaa san asana huku duniani watu
wakabadili kuwa ROHO MTAKATIFU ndio njiwa, hilo ni somo lingine tena, ila hapa
naelezea jinsi shetani kupitia roho wake mchafu ambaye anaitwa MAXWELL
aliwapoteza wanadamu wakabadili biblia na mpango wa YESU katika swala la
ubatizo, akawakosesha wanadamu ili wamkufuru ROHO MTAKATIFU na nafasi yake
ichukuliwe na mwanadamu.
Nawaeleza mimi Nabii Hebron sababu nawapenda, msiangamie, na
najua ipo adhabu iliyoandaliwa kwa watu watakaomkufuru ROHO MTAKATIFU ikiwemo
moja wapo ni wanadamu wanaosimamia watu ubatizo, nikuulize swali wewe ni ROHO
MTAKATIFU? Jibu, siyo. Sasa nani kakuloga ukakubali uchukue nafasi ya ROHO
MTAKATIFU? Jibu ni mafundisho ya mpinga kristo na makanisa yake ili na wewe
uangamie. Wengi wanayo iyo dhambi lakini hawajijui ni wenye dhambi na hata hao
wanaobatiza na kwa nini mtu awe na msimamizi na yeye ni mwenye dhambi vile vile
anayeshiriki kusimamia na kuhakikisha ROHO MTAKATIFU anatukanwa na shetani
anainuliwa katika dunia hii.
YESU aliponituma kwa watu wote aliniambia mengi na
aliniambia watumishi wamemsaliti ndio sababu wanadamu wanateseka ila sasa nenda
wewe Hebron nipo na wewe. Sema kweli yangu ili watu wapone, wanafikiri wapo
salama kumbe 98% ilishaangamia. Hebron ninarudi ila ni watu wachache sana ndio
wapo na mimi, 98% ni ya shetani na katika 98% wengi hawajui kama wameshatekwa
na shetani. 45% ya watumishi wote katika ulimwengu wote ni wachawi kwa kiwango
cha juu sana karibia wangefanana na shetani ila ni wanadamu. Ni marufuku kuchukua
utukufu wa ROHO MTAKATIFU enyi wamama wa ubatizo au wababa wa ubatizo
mnafanyika kuwa adui wa MUNGUmnaposhiriki na mnasimama badala ya shetani na
hata huo ubatizo ni wa kishetani sababu haujatoka mbinguni. Kila aliyesimamia
ubatizo atubu na atakayeendelea kusimamia ajielewe anamuinua shetani na huko
ndiko kumtukana MUNGU, yakupasa uelewe kuanzia sasa usishiriki kuwa baba wa
ubatizo, mama, kaka, babu, mjomba na wengineo, unatengenezewa kaburi na moto wa
milele ili ile siku ya mwisho uangamie na roho mchafu ambaye alifanikiwa kukutumia
mwili wako ili usimamie kama wewe ndio ROHO MTAKATIFU na uingie katika orodha
ya kuhukumiwa.
Sasa sema BWANA YESU naomba unisamehe nikijua au sikujua
nikawa msimamizi wa ubatizo tena hata huo ni machukizo sababu haukutoka kwako,
ulitokea kwa wanadamu ili watu wasiwe wana wa MUNGU, nimejua ukweli ninatubu
YESU, uniongoze na mimi nikabatizwe na unitenge na mahali pa ibada kama hizi na
wasimamizi wa ubatizo, wanadamu wa kumkufuru ROHO MTAKATIFU. Sitaki tena na
sitashiriki tena uchafu huo wa shetani. Amen.
Ukristo wenye asili ya kuzimu ndio wenye mapando ya wanadamu
na kulibadilisha neno kwa njia hiyo hata unayeshiriki kama msimamizi wa ubatizo
kama mwanadamu uelewe unayo mbegu ya ukristo wa kuzimu na MUNGU hakujui sababu hata Kristo aliyopo mbinguni
na yeye hakusimamiwa na mtu. Sasa uelewe kuwa ni upofu shetani aliwapiga watu
kupitia roho wa kristo wa kuzimu ili kuwateka wanadamu wawe ni wakristo ambao
ni wa kuzimu pasipo kujua kwa njia hiyo. Utakapotubu ndipo utakuwa mkristo wa
mbinguni na usirudi katika mapango hayo au hekalu sababu huko ni mahali pa
kristo wa kuzimu na wewe ukienda tena unatekwa tena.
NABII HEBRON.